Watu likawatishia, nje, ndani walokuwa,
Usalama hupotea, maafa mkahofia,
Treni bila dereva, lazima kuacha njia !
Na ndani unapokaa, budi kutazama njia,
Treni bila dereva, lazima kuacha njia !
Treni bila dereva, lazima kuacha njia !
Kona ukazitambua, na harari zilokuwa,
Ovyoovyo kijiendea, watu utaparamia,
Treni bila dereva, lazima kuacha njia !
Vilima usipojua,na mteremko ya njia,
Huangusha mabehewa, kilio kikubwa kuwa,
Vyuma vikajichimbia, na vingi kujipindia,
Treni bila dereva, lazima kuacha njia !
Dereva anatakiwa, chombo kukihudumia,
Njiani kujipitia, wote salama wakawa,
Vingine inapokuwa, uhai twauchezea,
Treni bila dereva, lazima kuacha njia !
Wapo wakudandia, na rafiki walokuwa,
Usije kuwaachia, bure wakajipandia,
Au za hongo wakanunua, tiketi zio bandia,
Treni bila dereva, lazima kuacha njia !
Hasara utaingia, shirika kuja jifia,
Kitambo ukiridhia, milele hudidimia,
Dunia hutuchezea, mitihani tulopewa,
Treni bila dereva, lazima kuacha njia !
Mawasiliano kivia, vingine hautajua,
Nyingine weza ingia, kwa mambo ya kusikia,
Hatari kubwa ikawa,kwa maisha na rupia,
Treni bila dereva, lazima kuacha njia !
Dereva atarajiwa, kazi moja kuifaa,
Nyingine akichukua, anaweza kuzidiwa,
Kija kutahamakia, mkenge mmeingia,
Treni bila dereva, lazima kuacha njia !
Safari yaashiria, dereva hatujamjua,
Na treni yakimbia, breki haijatiwa,
Sisi tunaposhangaa, wengine wachekelea ?
Treni bila dereva, lazima kuacha njia !
No comments:
Post a Comment