Tuesday, March 27, 2012

NI KAMA VILE SILAHA ?

MAJIBWA wanaugua, kubweka kumepungua,
Mwizi amewanunua, kuiba awatumia,
Kazi yao kutumia, kuzalisha ni nazaa,
Ni wananchi si silaha, na raia si Slaa:
Chama watakiondoa!

Vibaya wanatumia, utusini waingia,
Aibu yawaishia, kinamama walokua,
Na madume nayo pia, kuzomea mazoea,
Ni wananchi si silaha, na raia si Slaa:
Chama watakiondoa!

Na uandishi ukiwa, ndiyo huu umalaya,
Daima naukataa, siingii tasnia,
Kiumbe kujatumia, kma vile changuoa,
Ni wananchi si silaha, na raia si Slaa:
Chama watakiondoa!

Uongo ukweli huwa, na kweli kunajisiwa,
Nyuso zao zinang'aa, fedha wanaposikia,
Na cheo kuahidiwa, japo wengi ni majuha,
Ni wananchi si silaha, na raia si Slaa:
Chama watakiondoa!

Wakubwa wanatambua, benki walizipakua,
Hazina wakazizoa, hata dhahabu kutoa,
Wevi sote tunawajua, wengine wasingiziwa,
Ni wananchi si silaha, na raia si Slaa:
Chama watakiondoa!

Chama chao chahofia, nyuma i ko n yuklia,
CHADEMA ina silaha, bora sana ilokuwa,
Maangamizi walia, yako njiani kutua,
Ni wananchi si silaha, na raia si Slaa:
Chama watakiondoa!

Ila ninawaambia siye atayewaua,
Ndimi zao zachafua, na h asira kututia,
Wananchi tulokuwa, na ukweli twaujua,
Ni wananchi si silaha, na raia si Slaa:
Chama watakiondoa!

Sisi zaidi Slaa, yetu yanavyochochewa,
Wazawa sasa Slaa, fisadi yaelekea,
Bahati haitakuwa, zukunfu kujiokoa,
Ni wananchi si silaha, na raia si Slaa:
Chama watakiondoa!

Wameshindwa kujivua, gamba l ililochakaa,
Mabati wameyatia, kutu yaliyoingia,
Tetenasi twahofia, kila atakayesogea,
Ni wananchi si silaha, na raia si Slaa:
Chama watakiondoa!

Uoza wakumbatia, hadi ndani umejaa,
Chama chanuka balaa, keshokutwa mtajua,
Vijana wanachezewa, na ahadi wamepewa,
Ni wananchi si silaha, na raia si Slaa:
Chama watakiondoa!

Ahadi tuanzojua, za uongo zimekua,
Kila pembe Tanzania, wananchi wanayajutia,
Uoza kuuchagua, uoza kwao hidaya,
Ni wananchi si silaha, na raia si Slaa:
Chama watakiondoa!

Msumari ninatia, uswahiba nauvua,
Ndilo nililoamriwa, na juu aliyekuwa,
Wa dhuluma kukataa, na wasafi kusifia,
Ni wananchi si silaha, na raia si Slaa:
Chama watakiondoa!

Saturday, February 25, 2012

Lugha ya watu mizizi

Nimeyaona Asia, Ulaya ni mazoea,
Lugha wanajivunia, hata kidogo wakiwa,
Nyengine kutotumia, ila nje wanapokuwa,
Lugha ya watu mizizi, ikikatwa mti hufa:
Au ikifukuliwa
Na pengine kung'olewa
Utamaduni huvia
Taifa lije lemaa
Asili ikapotea
Uvumbuzi nao pia
Watu wabakie kuwa
Vya wengine watumia
Pasiwe kitu kimoya
Wao wanachogundua!



Chao wanajivunia, bila ya kusimamiwa,
Na kisha waongezea, vya wengine kuvijua,
Ubingwa kujipatia, kwayo na yale ya dunia,
Lugha ya watu mizizi, ikikatwa mti hufa:
Au ikifukuliwa
Na pengine kung'olewa
Utamaduni huvia
Taifa lije lemaa
Asili ikapotea
Uvumbuzi nao pia
Watu wabakie kuwa
Vya wengine watumia
Pasiwe kitu kimoya
Wao wanachogundua!


Asili waangalia, urithi kutopotea,
Pia rahisi ikawa, watoto kujifunzia,
Lughani wakichipua, mengi sana huyajua,
Lugha ya watu mizizi, ikikatwa mti hufa:
Au ikifukuliwa
Na pengine kung'olewa
Utamaduni huvia
Taifa lije lemaa
Asili ikapotea
Uvumbuzi nao pia
Watu wabakie kuwa
Vya wengine watumia
Pasiwe kitu kimoya
Wao wanachogundua!


Leo hapa Tanzania, maneno yanapotea,
Ndege wetu kuwajua, wazima utawaumbua,
Sembese watoto kuwa, hawana wanalojua,
Lugha ya watu mizizi, ikikatwa mti hufa:
Au ikifukuliwa
Na pengine kung'olewa
Utamaduni huvia
Taifa lije lemaa
Asili ikapotea
Uvumbuzi nao pia
Watu wabakie kuwa
Vya wengine watumia
Pasiwe kitu kimoya
Wao wanachogundua!


Wanyama nao pia, wawili watatu wajua,
Samaki waliojaa, bahari nayo maziwa,
Wangapi watakwambia, majina waliyopewa?
Lugha ya watu mizizi, ikikatwa mti hufa:
Au ikifukuliwa
Na pengine kung'olewa
Utamaduni huvia
Taifa lije lemaa
Asili ikapotea
Uvumbuzi nao pia
Watu wabakie kuwa
Vya wengine watumia
Pasiwe kitu kimoya
Wao wanachogundua!


Miti na mingi mimea, hakuna anayejua,
Utacheka nakwambia, mjini ukiulizia,
Afadhali inakuwa, kijijini wanajua,
Lugha ya watu mizizi, ikikatwa mti hufa:
Au ikifukuliwa
Na pengine kung'olewa
Utamaduni huvia
Taifa lije lemaa
Asili ikapotea
Uvumbuzi nao pia
Watu wabakie kuwa
Vya wengine watumia
Pasiwe kitu kimoya
Wao wanachogundua!


Maumbo yake dunia, wengi utata hukuwa,
Bure utajisumbua, hakuna anayejua,
Na hawa wategemea, kitu kuja kuvumbua?
Lugha ya watu mizizi, ikikatwa mti hufa:
Au ikifukuliwa
Na pengine kung'olewa
Utamaduni huvia
Taifa lije lemaa
Asili ikapotea
Uvumbuzi nao pia
Watu wabakie kuwa
Vya wengine watumia
Pasiwe kitu kimoya
Wao wanachogundua!


Mizizi yake mmea, asili hutegemea,
Ndipo inapokuwa, kwa yote yanayokuwa,
Elimu ikiwa pia, muhimu kuzingatiwa,
Lugha ya watu mizizi, ikikatwa mti hufa:
Au ikifukuliwa
Na pengine kung'olewa
Utamaduni huvia
Taifa lije lemaa
Asili ikapotea
Uvumbuzi nao pia
Watu wabakie kuwa
Vya wengine watumia
Pasiwe kitu kimoya
Wao wanachogundua!


Watafeli nadharia, kwa lugha kutoijua,
Watoto kuwakandia, ya uongo yalokuwa,
Walimu kuwazulia, hata wasiyofikiria,
Lugha ya watu mizizi, ikikatwa mti hufa:
Au ikifukuliwa
Na pengine kung'olewa
Utamaduni huvia
Taifa lije lemaa
Asili ikapotea
Uvumbuzi nao pia
Watu wabakie kuwa
Vya wengine watumia
Pasiwe kitu kimoya
Wao wanachogundua!


Kiswahili kutumia, kufundisha nadharia,
Kwa undani kuelewa, yote yanayozungumziwa,
Haya wakishayajua, Kama China tutakuwa,
Lugha ya watu mizizi, ikikatwa mti hufa:
Au ikifukuliwa
Na pengine kung'olewa
Utamaduni huvia
Taifa lije lemaa
Asili ikapotea
Uvumbuzi nao pia
Watu wabakie kuwa
Vya wengine watumia
Pasiwe kitu kimoya
Wao wanachogundua!


Tuitenge nadharia, na lugha kufundishia,
Maabara kufungua, shuleni na vyuo pia,
Lugha kuzikazania, mbili tatu wakajua,
Lugha ya watu mizizi, ikikatwa mti hufa:
Au ikifukuliwa
Na pengine kung'olewa
Utamaduni huvia
Taifa lije lemaa
Asili ikapotea
Uvumbuzi nao pia
Watu wabakie kuwa
Vya wengine watumia
Pasiwe kitu kimoya
Wao wanachogundua!


Ndege wengi tutaua,kwa jiwe moja kutumia,
Sayansi wakaijua, na lugha kuzing'amua,
Hata Kiarabu pia, na Kichina kutumia,
Lugha ya watu mizizi, ikikatwa mti hufa:
Au ikifukuliwa
Na pengine kung'olewa
Utamaduni huvia
Taifa lije lemaa
Asili ikapotea
Uvumbuzi nao pia
Watu wabakie kuwa
Vya wengine watumia
Pasiwe kitu kimoya
Wao wanachogundua!


Mashariki inafaa, tuanze kuangalia,
Isiwe tunachelewa,
Wenzeetu wakatangulia,
Lugha yetu kujitia, lakini kutokutufaa,
Lugha ya watu mizizi, ikikatwa mti hufa:
Au ikifukuliwa
Na pengine kung'olewa
Utamaduni huvia
Taifa lije lemaa
Asili ikapotea
Uvumbuzi nao pia
Watu wabakie kuwa
Vya wengine watumia
Pasiwe kitu kimoya
Wao wanachogundua!


Viongozi watakiwa, uzito kuuchukua,
Wafanze kuyaamua, mapema inavyokuwa,
Nami sintoshangaa, wengine kutangulia,
Lugha ya watu mizizi, ikikatwa mti hufa:
Au ikifukuliwa
Na pengine kung'olewa
Utamaduni huvia
Taifa lije lemaa
Asili ikapotea
Uvumbuzi nao pia
Watu wabakie kuwa
Vya wengine watumia
Pasiwe kitu kimoya
Wao wanachogundua!


Kiingereza balaa, ujanja wanatumia,
Lugha yetu kuiua, na yao kuendlea,
Na sisi kamamajuha, mtegoni twaingia,
Lugha ya watu mizizi, ikikatwa mti hufa:
Au ikifukuliwa
Na pengine kung'olewa
Utamaduni huvia
Taifa lije lemaa
Asili ikapotea
Uvumbuzi nao pia
Watu wabakie kuwa
Vya wengine watumia
Pasiwe kitu kimoya
Wao wanachogundua!


Nyerere alianzia, lugha kasaliti pia,
Mwinyi alipofatia, naye akazainiwa,
Mkapa hakujitambua, wala hatajitambua,
Lugha ya watu mizizi, ikikatwa mti hufa:
Au ikifukuliwa
Na pengine kung'olewa
Utamaduni huvia
Taifa lije lemaa
Asili ikapotea
Uvumbuzi nao pia
Watu wabakie kuwa
Vya wengine watumia
Pasiwe kitu kimoya
Wao wanachogundua!


Kikwete asipojua, humo humo kufatia,
Kiswahili kukiua, na elimu nayo pia,
Ndicho kilichobakia, na ndiyo yanayotokea,
Lugha ya watu mizizi, ikikatwa mti hufa:
Au ikifukuliwa
Na pengine kung'olewa
Utamaduni huvia
Taifa lije lemaa
Asili ikapotea
Uvumbuzi nao pia
Watu wabakie kuwa
Vya wengine watumia
Pasiwe kitu kimoya
Wao wanachogundua!


Ila mtunzi najua, rais wa Tanzania,
Kweli atakayekuwa, Kiswahili ataamua,
Kila ngazi kutumia, na nchi ikaendelea,
Lugha ya watu mizizi, ikikatwa mti hufa:
Au ikifukuliwa
Na pengine kung'olewa
Utamaduni huvia
Taifa lije lemaa
Asili ikapotea
Uvumbuzi nao pia
Watu wabakie kuwa
Vya wengine watumia
Pasiwe kitu kimoya
Wao wanachogundua!


Kwenye kapu watupiwa, wote waliotangulia,
Takataka watakuwa, kati yetu historia,
Nafasi waliipewa, ila hawakuitumia,
Lugha ya watu mizizi, ikikatwa mti hufa:
Au ikifukuliwa
Na pengine kung'olewa
Utamaduni huvia
Taifa lije lemaa
Asili ikapotea
Uvumbuzi nao pia
Watu wabakie kuwa
Vya wengine watumia
Pasiwe kitu kimoya
Wao wanachogundua!


Kuthubutu hapakua, na kujaribu wapwaya,
Hakuna walilojaliwa, kuliweza na kujua,
Waigaji wabakia, ni wasanii bandia,
Lugha ya watu mizizi, ikikatwa mti hufa:
Au ikifukuliwa
Na pengine kung'olewa
Utamaduni huvia
Taifa lije lemaa
Asili ikapotea
Uvumbuzi nao pia
Watu wabakie kuwa
Vya wengine watumia
Pasiwe kitu kimoya
Wao wanachogundua!

Unajifanya usilokuwa ?


Haukuwa na hatuokuwa

Ijapo nafasi ulishaipewa

Kiumbe jema hukujaliwa

Ila mabaya umeumbiwa

Shetani amekuchukuwa

Kama kifaa unatumiwa

Naye si rahisi ukajaliwa

Minyororoni ukajitowa

Yawa kama umelaniwa

Kwa pako pema kukimbiwa

Ukakimbilia kwenye mabaya!

Wajifanya usilokuwa

Nuksi hapo ndio zaanzia!


Umeme unapozima


Kwenye nchi ya madoa, rangi tusiyoyajua,

Na amri za kuua, wadhani hawajaua,

Na yatakiwayo kuwa, yasiwe yenye kukua,

Umeme unapozima, na giza likaenea:

Mwangaza hunifunua,

Utunzi nikaingia,

Hadi adhana ikawa!

Ukuu wanaochukua, wasiwe pakuanzia,

Na wanaoyachimbua, wakadhani walimia,

Huwa nchi ya wafukua, kuzikwa kwao haijawa,

Umeme unapozima, na giza likaenea:

Mwangaza hunifunua,

Utunzi nikaingia,

Hadi adhana ikawa!

Ndipo saa wazijua, kizani kutususia,

Mengi yananipitia, pembeni nilipokaa,

Wasiojua wajua, ndiyo nchi imekuwa,

Umeme unapozima, na giza likaenea:

Mwangaza hunifunua,

Utunzi nikaingia,

Hadi adhana ikawa!

Hakuna wa kutumiwa, wote wataka tumia,

Kuvuna washangilia, kupanda wanakataa,

Wachache hupalilia, nao mimea hung'oa,

Umeme unapozima, na giza likaenea:

Mwangaza hunifunua,

Utunzi nikaingia,

Hadi adhana ikawa!

Nchi ya wasiojijua, na kwendako wapotea,

Taifa lisilojifua, kutakata haijawa,

Na uchafu waujua, tena wanautumia,

Umeme unapozima, na giza likaenea:

Mwangaza hunifunua,

Utunzi nikaingia,

Hadi adhana ikawa!

Watu wa kusaidiwa, wasiojisaidia,

Nchi yenye kununua, chake isichokizaa,

Ni nchi ya kulaniwa, mbele haitoendelea,

Umeme unapozima, na giza likaenea:

Mwangaza hunifunua,

Utunzi nikaingia,

Hadi adhana ikawa!

Nchi ya viguu na njia, haiwezi kutulia,

Yao wasiotatua, ya wengine wakavaa,

Ni ya kusikitikiya, na tena kuhurumiwa,

Umeme unapozima, na giza likaenea:

Mwangaza hunifunua,

Utunzi nikaingia,

Hadi adhana ikawa!

Ndio ninafurahia, umeme ukisinzia,

Huamka na kuzua, visa vya kuhadithia,

Kizazi kitachokuwa, haya kuja yaambaa,

Umeme unapozima, na giza likaenea:

Mwangaza hunifunua,

Utunzi nikaingia,

Hadi adhana ikawa!

Binadamu si mashine


Hukuumbwa mashine, binadamu nakwambia,

Wapaswa kujitambua, akili kuitumia,

Watu wakikutumia, unakuwa ni kifaa,

Binadamu si mashine, apaswa kufikiria!


Itihari kajaliwa, kupima na kuchagua,

Afanye linalofaa, muktadha kuujua,

Na haki kuzingatia, kazini anapokuwa,

Binadamu si mashine, anapaswa kuchagua!

Ubongo kazawadiwa, apaswa kuutumia,

Na akishajipimia, mwenyewe akaamua,

Kwa vigezo vilokuwa, na watu na matukio,

Binadamu si mashine, anapaswa kuamua!


Vinginevyo ni bandia, mwanasesere akawa,

Wawe wamchezea, juu walotangulia,

Dhambi kumuachia, mwenyewe kujibebea,

Binadamu si mashine, apaswa kufikiria!

Wanasiasa balaa, fani yao yalaniwa,

Watu shere watezea, kama taahira wawa,

Ikawa wawakubalia, hata kwa yasiyokuwa,

Binadamu si mashine, anapaswa kuchagua!


Enzi zimeshaingia, watu kujiangalia,

Uhuru wakachagua, na haki kuzingatia,

Pasiwe wa kutumiwa, hadaa na kuzainiwa,

Binadamu si mashine, anapaswa kuamua!

Usitende bila fikra


Mnyama ungelikuwa, sawa tungelidhania,

Mambo kutofikiria, na kisha ukayaingia,

Utu yende kukuvua, na uchi ukabakia,

Usitende bila fikra, waza kabla kutenda!


Fikra ni majaliw,a mja amezawadiwa,

Yafaa kufikiria, kabla haujaamua,

Na utenzi hutanguliwa, kwa mawazo yalokuwa,

Usitende bila fikra, waza kabla kutenda!


Amri kuzipokea, ukatenda usojua,

Wewe umelaaniwa, na mbingu na ardhi pia,

Na moto wa kungojea, hunalo la kujitetea,

Usitende bila fikra, waza kabla kutenda!


La haki lililokuwa, kulitenda inafaa,

Na haki lisilokuwa, ni wajibu kukataa,

Muogopeni Jalia, si watu kuwahofia,

Usitende bila fikra, waza kabla kutenda!

Watu wao wapigao

Ni wale tuwajuao, nao ni kawaida yao,

Ukubwa wautakao, wale wao na wakwao,

Walinzi wafugwao, kulinda wakubwa wao,

Watu wao wapigao, si amani watakao!

Hudhani wao ni wao, na nchi hii ni yao,

Katiba wapinduao, juu kujiweka wao,

Na wananchi walalao, wakawa nalo pumbao,

Watu wao wapigao, si amani watakao!

Wasijue kuwa wao, ndio wao wafukuzao,

Asibaki mmojawao, zahama ikija kwao,

Uwe ni mwisho wao, na mwanzo wa wajuao,

Watu wao wapigao, si amani watakao!

Sauti ni nyie mnayo, na mambo muamuoa,

Mkitaka watoke wao, kutoka lazima kwao,

Isiwe ni warudio, juu tena sio yao,

Watu wao wapigao, si amani watakao!

Ni nyie muwawekao, na muamalizao,

Kwa lenu moja amuo, watoke hapo si kwao,

Wako wengi wenzao, nafasi waitakayo,

Watu wao wapigao, si amani watakao!

Haitoshi wajivuao, gamba liozalo kwao,

Na ngozi yenye kumbao, mwilini wabakiayo,

Uchago hulia wao, waulaliapo mwao,

Watu wao wapigao, si amani watakao!

Naamba niwaambiao, nyakati hizi si zao,

Mabadiliko ni ngao, huvunjika zao tao,

Yajayo si wazuiayo, watatoka watokao,

Watu wao wapigao, si amani watakao!

Kivumbasi mwanakwao, heri si wajaliwao,

Shetani ana kikao, mara kwa mara nao,

Na haya waamuayo, mwayaona yazuayo,

Watu wao wapigao, si amani watakao!

Urithi si watakao, wawapa kwanza wanao,

Kuua ni jadi yao, na wala sio wazaao,

Mti hujazaa mbao, si mbao yenye uzao,

Watu wao wapigao, si amani watakao!