Saturday, January 7, 2012

Muua demokrasia, si rafiki wa mwananchi!

WAFUASI wenye njaa, chama wanapokimbia,
Kwa mkubwa kuwanunua,kwingine anayetokea,
Wananchi bora kujua,demokrasia huua,
Muua demokrasia, si rafiki wa mwananchi!

Ukiritimba azua, uzidi kutusumbua,
Ubora unaovia, na nchi ikapotea,
Tuonekane vichaa, katika hii dunia,
Muua demokrasia, si rafiki wa mwananchi!

Hii ni hovyo ruia, wangapi kuwanunua?
Wenyewe watuibia, kisha wanatununua?
Naona tumeshapagawa, kama tunayavumilia,
Muua demokrasia, si rafiki wa mwananchi!

Ushindani watakiwa, mambo yetu bora kuwa,
Huyo anayekataa, udhaifu artwachia,
Kila tunapokomaa, mkengeni huishia,
Muua demokrasia, si rafiki wa mwananchi!

No comments: