Kuishi usiyejua, nini kesho wajiia,
Riziki kungojea, ya sadaka kugawiwa,
HIVI huu ni udini, au yatokota njaa ?
Kuishi usiyejua, mwana vipi wamlea,
Kwa karamu kungojea, tajiri kumpikia,
Makombo ukachukua, wana kuja walishia,
Hivi vitu si mabomu, njaa na umaskini !
Kushi bila kujua, ni mtumwa wa majaa,
Ukafiri ukatiwa, kwa sharti za kupewa,
Utaikifu dunia, uchafu ukishajaa,
Hivi vitu si mabomu, ajira kukosekana?
Matambara utakuwa, na mitumba wa kuvaa,
Huku unajionea, yako yakipakuliwa,
Mtupu ukaachiwa, maganda umeshakuwa,
Hivi vitu si mabomu, ujinga na kununuliwa?
Dira huwa zakataa, njia kutojionea,
Na kila ukifikiria, mbaya utamdhania,
Juu anayekukalia, kama jiko na mkaa,
Hivi vitu si mabomu, wongo na udanganyifu?
Kisha hukusimuliwa, na ukweli yasokuwa,
Nawe akutarajia, hayo utamkubalia,
Kingine ukisikia, uongo wende kulia,
Zidini kutuibia, mola atatufidia!
Majira yakiwadia, joho hili hujivua,
Yako ukaangalia, si ya wengine kujua,
Pasiwe wa kukumbatiwa, ila haki mwanadawa,
Zidini kutuibia, mola atatufidia!
No comments:
Post a Comment