Saturday, May 5, 2012
Lengo kuu kidunia
Imepwaya jumuiya, katika hii dunia,
Ovyoovyo twatembea, hata haramu kuvua,
Na kila ukiangalia, dini tunaichezea,
Lengo kuu kidunia, hatuna twababaika !
Angalia Tunisia, huko yaliyotokea,
Kisha ikafuatia, ya Gaddafy Libya,
Masri na Syria, sasa yanaendelea,
Lengo kuu kidunia, hatuna twababaika !
Kwingineko Indonesia, nako pia Malaysia,
Na zile za Kijamaa, Urussi zilizokua,
Kila ukiangalia, madhambi yawazidia,
Lengo kuu kidunia, hatuna twababaika !
Uchamungu wafulia, kisha bado wanalia,
Machafu wayaachia, nchini yanaingia,
Neema wazikataa, mgeni kuabudia,
Lengo kuu kidunia, hatuna twababaika !
Nasi tulishaambiwa, Miungu yao kuwaachia,
Wetu mmoya radhia, Azizi kuabudia,
Shiriki aikataa, na hili tunalijua,
Lengo kuu kidunia, hatuna twababaika !
Trela yaendelea, sinema haijaanzia,
Tsunami zaingia, kwa kushsto na kulia,
Na mioto naiwazia, siku ikijafikia,
Lengo kuu kidunia, hatuna twababaika !
Mengi sana yatavia, ukame ukijatokea,
Na kisa kuabudiwa, watu wanaozaliwa,
Tukaacha jitambua, Muumba kumhofia,
Lengo kuu kidunia, hatuna twababaika !
Iko siku tutalia, sio mbali nadhania,
Ukame ukiingia, na njaa ikasambaa,
Kisiote cha kufaa, na wanyama kujifia,
Lengo kuu kidunia, hatuna twababaika !
Viongozi wayajua, waliokijifanyia,
Hawana wa kusingizia, hukumu ikiwadia,
Ukimya waliokaa, hofu nyingi wanitia,
Lengo kuu kidunia, hatuna twababaika !
Ukimya waliokaa, hata wale wa dini pia,
Siwezi kuja shangaa, adhabu ikizidia,
Na mimi kusamehewa, sithubutu kujiombea,
Lengo kuu kidunia, hatuna twababaika !
Ni mmoja nimekuwa, kwa kushindwa kujijua,
Mapema ningewaambia, labda mngefikiria,
Makosa ninatubia, afu siwezi kataa,
Lengo kuu kidunia, hatuna twababaika !
Hivi vyote vya dunia
Hivi vyote vya dunia, huanza na kuishia,
Na wanaozuzuliwa, kubaya waelekea,
Muda ukishawadia, hana la kujitetea,
Hivi vyote vya dunia, vina mwanzo, vina mwisho!
Vitu vinatuzuzua, na watu watununua,
Hadhi yetu kitumbua, ughali hatujaujua,
Sinema yetu dunia, kwingine hatujaangalia,
Hivi vyote vya dunia, vina mwanzo, vina mwisho!
Ombwe tunapigania, kesho lisilotufaa,
Na madeni twanunua, tena kwa kujiaminia,
Siku hiyo kuyavua, mbona kazi itakuwa,
Hivi vyote vya dunia, vina mwanzo, vina mwisho!
Majumba twayalilia, japo ukweli twajua,
Kaburi haitakuwa, mita mraba kadhaa,
Huko kwa sana kukaa, hadi kuja fufuliwa,
Hivi vyote vya dunia, vina mwanzo, vina mwisho!
Magari twakimbilia, kumbe twaenda jiua,
Vikorokoro vyajaa, hata visivyotufaa,
Kila ukiangalia, naona hatujajijua,
Hivi vyote vya dunia, vina mwanzo, vina mwisho!
Shughuli twafatilia, thawabu zisikotiwa,
Na mengi kushangilia, yakuja kuugulia,
Siku iwe waangalia, huku unajililia,
Hivi vyote vya dunia, vina mwanzo, vina mwisho!
Ukweli twauhadaa, uongo twashikilia,
Islamu wabaya, watu wanatuhofia,
Na wengine walokuwa, ndugu wanawazulia,
Hivi vyote vya dunia, vina mwanzo, vina mwisho!
Twatendeana ubaya, kamab tumeiachia,
Unafiki wachanua, kila kona wajiotea,
Na dini yahujumiwa, na wanaonunuliwa,
Hivi vyote vya dunia, vina mwanzo, vina mwisho!
Kisirani imekua, maabadi yahofiwa,
Waweza kulipuliwa, mbali ukajifilia,
Na hii siyo hidaya, ni laana nahofia,
Hivi vyote vya dunia, vina mwanzo, vina mwisho!
Hakuna aliye mbora
Hakuna aliye bora, ila mwenye ucha Mungu,
Zenu kukuru kakara, mwisho wake ni mawingu,
Mawazo ya kifukara, yanawatia kiwingu,
Hakuna aliye mbora, zaidi ya Mchamungu!
Kwanini mnadorora, mwaishia ya mvungu,
Hazifani zenu sura, hudhani mwapigwa rungu,
Yawaishia stara, kwa kuzunguka mizungu,
Hakuna aliye mbora, zaidi ya Mchamungu!
Na wanaojiona bora, sawasawa na mabungu,
Hupaa kwenye ziara, wakirudi ni utungu,
Huishia kudorora, wakayakumba machungu,
Hakuna aliye mbora, zaidi ya Mchamungu!
Nayaomba maghufira, ukumbi huu si wangu,
Sijaiona bishara, kupata mradi wangu,
Nami si mwenye kuchora, nikala hata vya wenzangu,
Hakuna aliye mbora, zaidi ya Mchamungu!
Naikubali kudura, haya i usoni mwangu,
Kama chungu ninagura, na wangu pia mkungu,
Na wala sina harara, hulingoja langu fungu,
Hakuna aliye mbora, zaidi ya Mchamungu!
Ufukara wa mawazo
Ni mkubwa umasikini, kama fedha huna ndani,
Ila mie naamini, upo nisioutamani,
Na huu sio mgeni, naanika hadharani,
Ufukara wa mawazo, hakika unanitisha !
Siogopi umaskini, wala sijioni duni,
Ila niko mashakani, pasipo kitu kichwani,
Hujiona hayawani, na wala sijithamini,
Ufukara wa mawazo, hakika unanitisha !
Unatisha kwa yakini, wa mawazo umaskini,
Huwa kama afkani, taahirra majinuni,
Mtu huwezi jiamini, daima kuwa taabani,
Ufukara wa mawazo, hakika unanitisha !
Nauogopa amini, na katu siutamani,
Bora kingine yakini, huwa kwangu uhaini,
Nitakimbia jangwani, iwe watu siwaoni,
Ufukara wa mawazo, hakika unanitisha !
Usikatishe udugu
Udugu usikatishe, kwa kutokuelewana,
Damu msiikatishe, eti tu kwa kuzozana,
Kufaana msiishe, mtakuja kumbukana,
Usikatishe udugu, kwa kutokuelewana!
Mwenzie umsemeshe, hata mnapogombana,
Kisha basi na yaishe, na radhi mkatakana,
Udugu msikatishe, hilo hapendi Rabana,
Usikatishe udugu, kwa kutokuelewana!
Pengine mgonganishwe, na wagomvi wenu wa jana,
Ya uongo wayazushe, ili nyie mkagombana,
Haiwi mjjikaushe, haya mkaja yaona,
Usikatishe udugu, kwa kutokuelewana!
Watu wasiwawabaishe, nyie budi kuzikana,
Hata wawagombanishe, budi kuja elewana,
Acheni wakorofishe, yao kwao kutofichana,
Usikatishe udugu, kwa kutokuelewana!
Hadharani msibishe, waacheni kutoona,
Na nyie mjivishe, kama nanyi ni watwana,
Waacheni nje wakeshe, huku yenu mwayabana,
Usikatishe udugu, kwa kutokuelewana!
Nendeni mjipumzishe, msije kuumizana,
Na pumzi mzishushe, shetani kuondokana,
Huja vurugu ziishe, na ndugu mkaelewana,
Usikatishe udugu, kwa kutokuelewana!
Usiue urafiki
Sababu ya kosa moja, unaua urafiki,
Naona hiyo si hoja, au wacheza falaki,
Rafiki kubwa daraja, rahisi halibomoki,
Usiue urafiki, sababu ya kosa moja !
Ungeufunga mkaja, ujue lipi ni haki,
Na maneno ya waseja, haiwi yo yake laki,
Sahihi linalokuja, kuijali tawfiki,
Usiue urafiki, sababu ya kosa moja !
Ndio rojo yenye koja, haitaki unafiki,
Hainyewi kwa mrija, mdomo ndiyo yake haki,
Hakika mbili si moja, vingine haiaminiki,
Usiue urafiki, sababu ya kosa moja !
Tuesday, March 27, 2012
NI KAMA VILE SILAHA ?
MAJIBWA wanaugua, kubweka kumepungua,
Mwizi amewanunua, kuiba awatumia,
Kazi yao kutumia, kuzalisha ni nazaa,
Ni wananchi si silaha, na raia si Slaa:
Chama watakiondoa!
Vibaya wanatumia, utusini waingia,
Aibu yawaishia, kinamama walokua,
Na madume nayo pia, kuzomea mazoea,
Ni wananchi si silaha, na raia si Slaa:
Chama watakiondoa!
Na uandishi ukiwa, ndiyo huu umalaya,
Daima naukataa, siingii tasnia,
Kiumbe kujatumia, kma vile changuoa,
Ni wananchi si silaha, na raia si Slaa:
Chama watakiondoa!
Uongo ukweli huwa, na kweli kunajisiwa,
Nyuso zao zinang'aa, fedha wanaposikia,
Na cheo kuahidiwa, japo wengi ni majuha,
Ni wananchi si silaha, na raia si Slaa:
Chama watakiondoa!
Wakubwa wanatambua, benki walizipakua,
Hazina wakazizoa, hata dhahabu kutoa,
Wevi sote tunawajua, wengine wasingiziwa,
Ni wananchi si silaha, na raia si Slaa:
Chama watakiondoa!
Chama chao chahofia, nyuma i ko n yuklia,
CHADEMA ina silaha, bora sana ilokuwa,
Maangamizi walia, yako njiani kutua,
Ni wananchi si silaha, na raia si Slaa:
Chama watakiondoa!
Ila ninawaambia siye atayewaua,
Ndimi zao zachafua, na h asira kututia,
Wananchi tulokuwa, na ukweli twaujua,
Ni wananchi si silaha, na raia si Slaa:
Chama watakiondoa!
Sisi zaidi Slaa, yetu yanavyochochewa,
Wazawa sasa Slaa, fisadi yaelekea,
Bahati haitakuwa, zukunfu kujiokoa,
Ni wananchi si silaha, na raia si Slaa:
Chama watakiondoa!
Wameshindwa kujivua, gamba l ililochakaa,
Mabati wameyatia, kutu yaliyoingia,
Tetenasi twahofia, kila atakayesogea,
Ni wananchi si silaha, na raia si Slaa:
Chama watakiondoa!
Uoza wakumbatia, hadi ndani umejaa,
Chama chanuka balaa, keshokutwa mtajua,
Vijana wanachezewa, na ahadi wamepewa,
Ni wananchi si silaha, na raia si Slaa:
Chama watakiondoa!
Ahadi tuanzojua, za uongo zimekua,
Kila pembe Tanzania, wananchi wanayajutia,
Uoza kuuchagua, uoza kwao hidaya,
Ni wananchi si silaha, na raia si Slaa:
Chama watakiondoa!
Msumari ninatia, uswahiba nauvua,
Ndilo nililoamriwa, na juu aliyekuwa,
Wa dhuluma kukataa, na wasafi kusifia,
Ni wananchi si silaha, na raia si Slaa:
Chama watakiondoa!
Mwizi amewanunua, kuiba awatumia,
Kazi yao kutumia, kuzalisha ni nazaa,
Ni wananchi si silaha, na raia si Slaa:
Chama watakiondoa!
Vibaya wanatumia, utusini waingia,
Aibu yawaishia, kinamama walokua,
Na madume nayo pia, kuzomea mazoea,
Ni wananchi si silaha, na raia si Slaa:
Chama watakiondoa!
Na uandishi ukiwa, ndiyo huu umalaya,
Daima naukataa, siingii tasnia,
Kiumbe kujatumia, kma vile changuoa,
Ni wananchi si silaha, na raia si Slaa:
Chama watakiondoa!
Uongo ukweli huwa, na kweli kunajisiwa,
Nyuso zao zinang'aa, fedha wanaposikia,
Na cheo kuahidiwa, japo wengi ni majuha,
Ni wananchi si silaha, na raia si Slaa:
Chama watakiondoa!
Wakubwa wanatambua, benki walizipakua,
Hazina wakazizoa, hata dhahabu kutoa,
Wevi sote tunawajua, wengine wasingiziwa,
Ni wananchi si silaha, na raia si Slaa:
Chama watakiondoa!
Chama chao chahofia, nyuma i ko n yuklia,
CHADEMA ina silaha, bora sana ilokuwa,
Maangamizi walia, yako njiani kutua,
Ni wananchi si silaha, na raia si Slaa:
Chama watakiondoa!
Ila ninawaambia siye atayewaua,
Ndimi zao zachafua, na h asira kututia,
Wananchi tulokuwa, na ukweli twaujua,
Ni wananchi si silaha, na raia si Slaa:
Chama watakiondoa!
Sisi zaidi Slaa, yetu yanavyochochewa,
Wazawa sasa Slaa, fisadi yaelekea,
Bahati haitakuwa, zukunfu kujiokoa,
Ni wananchi si silaha, na raia si Slaa:
Chama watakiondoa!
Wameshindwa kujivua, gamba l ililochakaa,
Mabati wameyatia, kutu yaliyoingia,
Tetenasi twahofia, kila atakayesogea,
Ni wananchi si silaha, na raia si Slaa:
Chama watakiondoa!
Uoza wakumbatia, hadi ndani umejaa,
Chama chanuka balaa, keshokutwa mtajua,
Vijana wanachezewa, na ahadi wamepewa,
Ni wananchi si silaha, na raia si Slaa:
Chama watakiondoa!
Ahadi tuanzojua, za uongo zimekua,
Kila pembe Tanzania, wananchi wanayajutia,
Uoza kuuchagua, uoza kwao hidaya,
Ni wananchi si silaha, na raia si Slaa:
Chama watakiondoa!
Msumari ninatia, uswahiba nauvua,
Ndilo nililoamriwa, na juu aliyekuwa,
Wa dhuluma kukataa, na wasafi kusifia,
Ni wananchi si silaha, na raia si Slaa:
Chama watakiondoa!
Subscribe to:
Posts (Atom)