Thursday, May 30, 2013

Kila muabudu mtu


Wakizuka nakwambia, waabuduji wakawa,

Watu wawatangulia, na ibada kuwafanyia,

Tambua bado wazua, trela wameanzia,

Kila muabudu mtu, hutaka naye uungu!

 

 

Kichuguu wachukua, wao mlima walilia,

Mlango wa kupitia, lazima pa kuanzia,

Budi mtu  kuchezewa, kttu asiyetambua,

Kila muabudu mtu, hutaka naye uungu!

 

Wao wakajiandaa, uungu kuununua,

Wafanye ya kushtua, wakatingisha dunia,

Na uliyewaachia, ukaja kuyajutia,

Kila muabudu mtu, hutaka naye uungu!

 

Milango yafunguliwa, muda haujaishia,

Toba kuikimbilia, maghufira kiuyajua,

Ibilisi kumkataa, na mbali ukamlania,

Kila muabudu mtu, hutaka naye uungu!

 

Mtu wa kuabudiwa, apaswa awe raia,

Kwa shidaye kuijua, na  tatizo kutatua,

Hakika ninawaambia, Mola hapo mtamjua,

Kila muabudu mtu, hutaka naye uungu!

 

Vingine mwamchezea, hasiraye ikakua,

Kidogo kilichokuwa, mlima kugeuziwa,

Viumeb mwachanganyikiwa, si miaka mna saa,

Kila muabudu mtu, hutaka naye uungu!

No comments: