Saturday, February 25, 2012

Kumpanda mume la'na, na sasa unayaona!


Na nilikuangalia, na kutaka kukulea,

Mjinga kwako nikawa, na kubasi la kwogea,

Yangu uliyakataa, ya ngoroko kuchukua,

Kumpanda mume la'na, na sasa unayaona!

Jeui ukajitia, na matusi kukujaa,

Dharau ukaivaa, na shanga kuivalia,

Nami kimya nikakaa, siku nikiingojea,

Kumpanda mume la'na, na sasa unayaona!

Muda haukuchelewa, miaka ikafikia,

Uhuru ulipokuwa, na waoto wamekua,

Hukujua nangojea, ulidhani natania,

Kumpanda mume la'na, na sasa unayaona!

Ulikuwa ni kichaa, mtu usiyesikia,

Yako kujifanyia, yasiyowapendezea,

Na laana kufukua, na wana kuwatupia,

Kumpanda mume la'na, na sasa unayaona!

Mapenzi hukujaliwa, ila wabeba sanaa,

Kila kitu kujitia, wajua usiyejua,

Wengi wakakushangaa, ujinga uliovaa,

Kumpanda mume la'na, na sasa unayaona!

Juzuu kukazania, sasa unattakiwa,

Sura Na'ba kuijua, dua ukaiombea,

Maradhi kukupungua, kichwani yalokujaa,

Kumpanda mume la'na, na sasa unayaona!

Na jeneza kuzuia, wana lisije chukua,

Wazee wako yafaa, kinga kuwaulizia,

Upuuzi uliotoa, madhara kutotokea,

Kumpanda mume la'na, na sasa unayaona!

Ni mpweke nitakuwa, ila kensa naitoa,

Pengine nitafikiria, madeni ukilipiwa,

Nyumbani ukarejea, mama wa nyumbani kuwa,

Kumpanda mume la'na, na sasa unayaona!

Biashara nakataa, marufuku kuijua,

Ila vitu kuandaa, nyumbani unapokuwa,

Na mikopo kuchukua, si ruhusa nakwambia,

Kumpanda mume la'na, na sasa unayaona!

Wataka waharibia, wana wangali wakua,

Msingi kumalizia, chini wote kuishia,

Hakika wakosa haya, kisirani umekuwa,

Kumpanda mume la'na, na sasa unayaona!

Na jeuri wajitia, kujifanya waonewa,

Mwisho umeshafikia, ukweli tunaujua,

Wengi umewaibia, siku zote wanalia,

Kumpanda mume la'na, na sasa unayaona!

Nakuomba angukia, ndugu kukusaidia,

Mikopo uliyochukua, na wizi ulokuwa,

Madeni kukulipia, salama upate kuwa,

Kumpanda mume la'na, na sasa unayaona!

Dharau imekuponza


Na nilikuangalia, na kutaka kukulea,

Mjinga kwako nikawa, na kubasi la kuvua,

Yangu uliyakataa, ya ngoroko kuchukua,

Dharau imekuponza, sasa wajidhalilisha!

Jeui ukajitia, na matusi kukujaa,

Dharau ukaivaa, na shanga kuivalia,

Nami kimya nikakaa, siku nikiingojea,

Dharau imekuponza, sasa wajidhalilisha!

Muda haukuchelewa, miaka ikafikia,

Uhuru ulipokuwa, na waoto wamekua,

Hukujua nangojea, ulidhani natania,

Dharau imekuponza, sasa wajidhalilisha!

Ulikuwa ni kichaa, mtu usiyesikia,

Yako kujifanyia, yasiyowapendezea,

Na laana kufukua, na wana kuwatupia,

Dharau imekuponza, sasa wajidhalilisha!

Mapenzi hukujaliwa, ila wabeba sanaa,

Kila kitu kujitia, wajua usiyejua,

Wengi wakakushangaa, ujinga uliovaa,

Dharau imekuponza, sasa wajidhalilisha!

Juzuu kukazania, sasa unattakiwa,

Sura Na'ba kuijua, dua ukaiombea,

Maradhi kukupungua, kichwani yalokujaa,

Dharau imekuponza, sasa wajidhalilisha!

Na jeneza kuzuia, wana lisije chukua,

Wazee wako yafaa, kinga kuwaulizia,

Upuuzi uliotoa, madhara kutotokea,

Dharau imekuponza, sasa wajidhalilisha!

Ni mpweke nitakuwa, ila kensa naitoa,

Pengine nitafikiria, madeni ukilipiwa,

Nyumbani ukarejea, mama wa nyumbani kuwa,

Dharau imekuponza, sasa wajidhalilisha!

Biashara nakataa, marufuku kuijua,

Ila vitu kuandaa, nyumbani unapokuwa,

Na mikopo kuchukua, si ruhusa nakwambia,

Dharau imekuponza, sasa wajidhalilisha!

Wataka waharibia, wana wangali wakua,

Msingi kumalizia, chini wote kuishia,

Hakika wakosa haya, kisirani umekuwa,

Dharau imekuponza, sasa wajidhalilisha!

Na jeuri wajitia, kujifanya waonewa,

Mwisho umeshafikia, ukweli tunaujua,

Wengi umewaibia, siku zote wanalia,

Dharau imekuponza, sasa wajidhalilisha!

Nakuomba angukia, ndugu kukusaidia,

Mikopo uliyochukua, na wizi ulokuwa,

Madeni kukulipia, salama upate kuwa,

Dharau imekuponza, sasa wajidhalilisha!

Kiburi kimekuponza,

Na nilikuangalia, na kutaka kukulea,

Mjinga kwako nikawa, na kubasi la kuvua,

Yangu uliyakataa, ya ngoroko kuchukua,

Kiburi kimekuponza, mbona sasa unalia ?

Jeui ukajitia, na matusi kukujaa,

Dharau ukaivaa, na shanga kuivalia,

Nami kimya nikakaa, siku nikiingojea,

Kiburi kimekuponza, mbona sasa unalia ?

Muda haukuchelewa, miaka ikafikia,

Uhuru ulipokuwa, na waoto wamekua,

Hukujua nangojea, ulidhani natania,

Kiburi kimekuponza, mbona sasa unalia ?

Ulikuwa ni kichaa, mtu usiyesikia,

Yako kujifanyia, yasiyowapendezea,

Na laana kufukua, na wana kuwatupia,

Kiburi kimekuponza, mbona sasa unalia ?

Mapenzi hukujaliwa, ila wabeba sanaa,

Kila kitu kujitia, wajua usiyejua,

Wengi wakakushangaa, ujinga uliovaa,

Kiburi kimekuponza, mbona sasa unalia ?

Juzuu kukazania, sasa unattakiwa,

Sura Na'ba kuijua, dua ukaiombea,

Maradhi kukupungua, kichwani yalokujaa,

Kiburi kimekuponza, mbona sasa unalia ?

Na jeneza kuzuia, wana lisije chukua,

Wazee wako yafaa, kinga kuwaulizia,

Upuuzi uliotoa, madhara kutotokea,

Kiburi kimekuponza, mbona sasa unalia ?

Ni mpweke nitakuwa, ila kensa naitoa,

Pengine nitafikiria, madeni ukilipiwa,

Nyumbani ukarejea, mama wa nyumbani kuwa,

Kiburi kimekuponza, mbona sasa unalia ?

Biashara nakataa, marufuku kuijua,

Ila vitu kuandaa, nyumbani unapokuwa,

Na mikopo kuchukua, si ruhusa nakwambia,

Kiburi kimekuponza, mbona sasa unalia ?

Wataka waharibia, wana wangali wakua,

Msingi kumalizia, chini wote kuishia,

Hakika wakosa haya, kisirani umekuwa,

Kiburi kimekuponza, mbona sasa unalia ?

Na jeuri wajitia, kujifanya waonewa,

Mwisho umeshafikia, ukweli tunaujua,

Wengi umewaibia, siku zote wanalia,

Kiburi kimekuponza, mbona sasa unalia ?

Nakuomba angukia, ndugu kukusaidia,

Mikopo uliyochukua, na wizi ulokuwa,

Madeni kukulipia, salama upate kuwa,

Kiburi kimekuponza, mbona sasa unalia ?

Jeuri imekuponza

Na nilikuangalia, na kutaka kukulea,

Mjinga kwako nikawa, na kubasi la kuvua,

Yangu uliyakataa, ya ngoroko kuchukua,

Jeuri imekuponza, mwenyewe wajiumiza!

Jeui ukajitia, na matusi kukujaa,

Dharau ukaivaa, na shanga kuivalia,

Nami kimya nikakaa, siku nikiingojea,

Jeuri imekuponza, mwenyewe wajiumiza!

Muda haukuchelewa, miaka ikafikia,

Uhuru ulipokuwa, na waoto wamekua,

Hukujua nangojea, ulidhani natania,

Jeuri imekuponza, mwenyewe wajiumiza!

Ulikuwa ni kichaa, mtu usiyesikia,

Yako kujifanyia, yasiyowapendezea,

Na laana kufukua, na wana kuwatupia,

Jeuri imekuponza, mwenyewe wajiumiza!

Mapenzi hukujaliwa, ila wabeba sanaa,

Kila kitu kujitia, wajua usiyejua,

Wengi wakakushangaa, ujinga uliovaa,

Jeuri imekuponza, mwenyewe wajiumiza!

Juzuu kukazania, sasa unattakiwa,

Sura Na'ba kuijua, dua ukaiombea,

Maradhi kukupungua, kichwani yalokujaa,

Jeuri imekuponza, mwenyewe wajiumiza!

Na jeneza kuzuia, wana lisije chukua,

Wazee wako yafaa, kinga kuwaulizia,

Upuuzi uliotoa, madhara kutotokea,

Jeuri imekuponza, mwenyewe wajiumiza!

Ni mpweke nitakuwa, ila kensa naitoa,

Pengine nitafikiria, madeni ukilipiwa,

Nyumbani ukarejea, mama wa nyumbani kuwa,

Jeuri imekuponza, mwenyewe wajiumiza!

Biashara nakataa, marufuku kuijua,

Ila vitu kuandaa, nyumbani unapokuwa,

Na mikopo kuchukua, si ruhusa nakwambia,

Jeuri imekuponza, mwenyewe wajiumiza!

Wataka waharibia, wana wangali wakua,

Msingi kumalizia, chini wote kuishia,

Hakika wakosa haya, kisirani umekuwa,

Jeuri imekuponza, mwenyewe wajiumiza!

Na jeuri wajitia, kujifanya waonewa,

Mwisho umeshafikia, ukweli tunaujua,

Wengi umewaibia, siku zote wanalia,

Jeuri imekuponza, mwenyewe wajiumiza!

Nakuomba angukia, ndugu kukusaidia,

Mikopo uliyochukua, na wizi ulokuwa,

Madeni kukulipia, salama upate kuwa,

Jeuri imekuponza, mwenyewe wajiumiza!

Kuiga mambo ya watu

Akili hukutumia, ingwa umejaliwa,

Bahati ukachezea, chooni ulipokuwa,

Shilingi kutumbukia, vyote vimeshapotea,

Kufata watu wa nje, wa ndani ukawabeza:

Nyongo yakutumbukia!

Ya mme hukusikia, kiburi ukajitia,

Na jeuri ukawa, kila alipokuongoa,

Heri ukaikataa, na shari kukurubia,

Kufata watu wa nje, wa ndani ukawabeza:

Nyongo yakutumbukia!

Wa nje kuwaendea, shirika kujifanyia,

Na waganga kuzoea, ushirikina kujaa,

Mkawa mwachanganyikiwa, mwazidi potea njia,

Kufata watu wa nje, wa ndani ukawabeza:

Nyongo yakutumbukia!

Wakowapi walokua, kila siku wasifia,

Kidume uliyekuwa, mume chini yako kawa,

Kumbe akuhesabia, siku yako kufikia,

Kufata watu wa nje, wa ndani ukawabeza:

Nyongo yakutumbukia!

Sura ulipuuzia, ila dini wajitia,

Kurani hukuijua, ubishi ulikujaa,

Na ulichoambulia, mwenyewe unakijua,

Kufata watu wa nje, wa ndani ukawabeza:

Nyongo yakutumbukia!

Un afiki kujitia, na uswalihina pia,

Kumbe nyoka ulikua, kichinichini wajia,

Kutuchoma kuamua, nyumbani tulokaa,

Kufata watu wa nje, wa ndani ukawabeza:

Nyongo yakutumbukia!

Dunia yakuumbua, mwanamke wa balaa,

Haya hukuitambua, nani kukuangalia,

Mola ukimrudia, pengine kukuafua,

Kufata watu wa nje, wa ndani ukawabeza:

Nyongo yakutumbukia!

Ushirikina kimbia, au unaangamia,

Na mume kumwangukia, ndiyo dawa itakuwa,

Vinginevyo twachomoa, akhera mbali pia kuwa,

Kufata watu wa nje, wa ndani ukawabeza:

Nyongo yakutumbukia!

Dhuluma kujifanyia, na urushi kuujua,

Sumu yake hukujua, wanao itawavaa,

Wajukuu nao pia, usipowarejeshea,

Kufata watu wa nje, wa ndani ukawabeza:

Nyongo yakutumbukia!

Rahma ungelikuwa, haya yasingetokea,

Ila kwa kukosa neema, ulizaliwa Rehema,

Tubu kisha ungamia,

Kufata watu wa nje, wa ndani ukawabeza:

Nyongo yakutumbukia!

Starehe gani hii ?


Kila mtu ashangaa, dhiki waikimbilia,

Wengi wanavyodhania, pengine umechezewa,

Kulogwa inshakuwa, huu nusu ukichaa,

Starehe gani hii, dhiki kuikimbilia ?

Si bure umechezewa, au mzazi kachukia,

Mema unayotendewa, kwako ubaya inkuwa?

Wengine waililia, nafasi uliyopewa,

Starehe gani hii, dhiki kuikimbilia ?

Uhuru umegaiwa, wewe waudhihakia,

Unaibeza tabia, ya ulua wa kufaa,

Na uchafu wautwaa, mwilini kujimwagiwa,

Starehe gani hii, dhiki kuikimbilia ?

Huu kama ukichaa, naona ilivyokuwa,

Kila siku ikiingia, hali huwa kote mbaya,

Watu wanaulizia, kanyimwa na kupagawa?

Starehe gani hii, dhiki kuikimbilia ?

Wabaya washangilia, zuzu kusesembuliwa,

Raha waitamania, ije kuwaangukia,

Kila wakikazania, kofuli bado yatiwa,

Starehe gani hii, dhiki kuikimbilia ?

Lango langu kufungua, haijawa, nanuia,

Hadi akitokea, malaika atembea,

Urulaini radhia, duniani akajaa,

Starehe gani hii, dhiki kuikimbilia ?

Mazuri wayaachia, mabaya wang'ang'ania,

Nini kinakuzuzua, bado hatujakijua,

Kila pembe twaulizia, majibu hatujapewa,

Starehe gani hii, dhiki kuikimbilia ?

Mtaji umeitwaa, nani kukusaidia,

Wazazi nini kupewa, hali pato umeua?

Wallahi nakusikitia, ninatamani kulia,

Starehe gani hii, dhiki kuikimbilia ?

Raha uliidhania, nje utajiokotea,

Ndani ukapachukia, na wa ndani kuwa udhia,

Laiti ungelijua, ndani ungejiangalia,

Starehe gani hii, dhiki kuikimbilia ?

Siachi kukusetiri

Islamu twaambiwa, ya wenzetu kutotoa,

Na mini nakuambia, yako ninahifadhia,

Isipokuwa yalokuwa, nje ya uwezo kuwa,

Siachi kukusetiri, na mini nisetiriwa:

Ila ya wabaya wako, watu lazima kujua,

Hadi radhi kuitoa,

Wakupe na msamaha!

Yako nitakufichia, wengine kutoyajua,

Ila nje uliyotoa, siwezi kuyazuia,

Aibu yako ikawa, mimi haukunambia,

Siachi kukusetiri, na mini nisetiriwa:

Ila ya wabaya wako, watu lazima kujua,

Hadi radhi kuitoa,

Wakupe na msamaha!

Vya watu ulivyotwaa, kurudisha watakiwa,

Laana kutoachiwa, wana wasio hatia,

Mama mpenda familia, hagtotaka kuumia,

Siachi kukusetiri, na mini nisetiriwa:

Ila ya wabaya wako, watu lazima kujua,

Hadi radhi kuitoa,

Wakupe na msamaha!

Watoto unatakiwa, kheri wapate zawadiwa,

Mama kutokuingia, kwenye maovu ya dunia,

Mwenyezi kumrudia, tawba hataoikataa,

Siachi kukusetiri, na mini nisetiriwa:

Ila ya wabaya wako, watu lazima kujua,

Hadi radhi kuitoa,

Wakupe na msamaha!

Shetani alokwingia, pengine atamtoa,

Kawaida kurejea, ibilisi kumwambaa,

Na zako hawa jamaa, salama wakatunukiwa,

Siachi kukusetiri, na mini nisetiriwa:

Ila ya wabaya wako, watu lazima kujua,

Hadi radhi kuitoa,

Wakupe na msamaha!

Nami ninakuombea, tobayo kukubaliwa,

Na rehema ukapewa, na msamaha maridhawa,

Ukaijali familia, pamoja tukarejea,

Siachi kukusetiri, na mini nisetiriwa:

Ila ya wabaya wako, watu lazima kujua,

Hadi radhi kuitoa,

Wakupe na msamaha!