Saturday, May 5, 2012
Ndugu zetu Waarabu
Nimekuja kugundua, ahali sikuwajua,
Ila walotulalia, akili kutuchezea,
Hadi kuwaabudia, na sasa tunapotea,
Ndugu zetu Waarabu, na wala sio wazungu !
Damu nimeigundua, kila pembe yaenea,
Dini waliichukia, mpya na asilia,
Nasara wakavamia, athari kuziondoa,
Ndugu zetu Waarabu, na wala sio wazungu !
Ila hawakujaliwa, ulinzi umebakia,
Mwenyewe kaangalia, hadi leo kufikia,
Haifai kumwachia, uamsho watakiwa,
Ndugu zetu Waarabu, na wala sio wazungu !
Hapa linalokusudiwa, dini yetu kurejea,
Huku tunajitambua, Kiswahili tulipewa,
Vyama tukikitumia, mbali sana tutapaa,
Ndugu zetu Waarabu, na wala sio wazungu !
Vyuo mnangojewa, kuja kujianzishia,
Elimu ikaitoa, kwa lugha pacha zikawa,
Kiswahili na Arabia, tulivyokwishajaliwa,
Ndugu zetu Waarabu, na wala sio wazungu !
Vyuo vikuu pia, lugha kuzifundishia,
Hadi dokta wakawa, ndugu zetu Tanzania,
Na kisha kufuatia, Afrika ikapaa,
Ndugu zetu Waarabu, na wala sio wazungu !
Themanini kwayo mia, ni yake asilimia,
Maneno Kiarabia, Kiswahii imetwaa,
Hili ukizingatia, lugha kujua inafaa,
Ndugu zetu Waarabu, na wala sio wazungu !
Gele wanatuonea, Wahausa Nigeria,
Kama wao wangekuwa, hatua wangeshachukua,
Na mazuri yakajaa, na wala sio balaa,
Ndugu zetu Waarabu, na wala sio wazungu !
Kitu hatujapungukiwa, yabaki kuzitumia,
Unyonge tukajivua, na asili kuringia,
Kiingereza kitapwaya, wallahi nawaambia,
Ndugu zetu Waarabu, na wala sio wazungu !
Ndugu zetu twawajua, umoja tunatakiwa,
Yetu kuja fanikiwa, kitu kimoja i dua,
Vingine tukiachia, lazima tutahujumiwa,
Ndugu zetu Waarabu, na wala sio wazungu !
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
No comments:
Post a Comment