Monday, August 26, 2013
BARUA
Barua nimepokea, pasina kujitambua,
Jina nishaling'amua, langu wala haikuwa,
Maudhui nashangaa, ni jambo nisilojua,
Barua uliyotuma, haikuwa na anwani !
Raha nilijisikia, namiye kuandikiwa,
Japo sikumtambua, aliyeniandikia,
Kusoma nikajitia, kwa juhudi kuuvmbua,
Barua uliyotuma, haikuwa na anwani !
Wallahi sikudadavua, wala kitu kutambua,
Ila nimechanganyikiwa, asili nisiyoijua,
Na sasa najiinamia, kuwaza na kuwazua,
Barua uliyotuma, haikuwa na anwani !
Dhamira sijaijua, wala lililokusudiwa,
Lengo sijalitambua, ramli sikujaliwa,
Kichwa ninaugulia, yote nataka kujua,
Barua uliyotuma, haikuwa na anwani !
Utata unenijaa, nasibu naichezea,
Geresha ingelikuwa, nia sijaitambua,
Mengine kuyang'amua, subira yahitajiwa,
Barua uliyotuma, haikuwa na anwani !
Mwanga ninaungojea, hili kuja niangazia,
Pengine nitagundua, japo palipoanzia,
Kisha nikaendelea, kufuma na kufumua,
Barua uliyotuma, haikuwa na anwani !
MTU MWEMA
Shetani keshajitoma, ndaniyo ametulia,
Dhamiri tokea zama, yako kkutibulia,
Ukaikimbia njia, ya uzima pia twaha,
Mtu mwema kumuiza, huhamia ibilisi !
Shetani akuhadaa, kuona bora dunia,
Sasa wamtumikia, pasina kujitambua,
Serikali ilokuwa, Mola inamkataa,
Mtu mwema kumuiza, huhamia ibilisi !
Shere inamfanzia, aliyeumba dunia,
Wao juu wamekuwa, na uchungi wakataa,
Milango waiachia, ibilisi kujimwaa,
Mtu mwema kumuiza, huhamia ibilisi !
Mtu tunamhofia, Mola tunamchezea?
Subira kaichagua, twasema amefulia ?
Yaja tusiyoyajua, kizazi tualilia,
Mtu mwema kumuiza, huhamia ibilisi !
Ibada twazikimbia, sherehe kuziwania,
Muda ametuachia, tawba kuirejea,
Unguja na Tanzania, huruma ninawaonea,
Mtu mwema kumuiza, huhamia ibilisi !
Kitabu twakitania, na dini kuifukia ?
Kati yetu sijajua, nani alokuwa juha,
Ya miezi twaridhia, ya karne twaachia?
Mtu mwema kumuiza, huhamia ibilisi !
Dhamiri tokea zama, yako kkutibulia,
Ukaikimbia njia, ya uzima pia twaha,
Mtu mwema kumuiza, huhamia ibilisi !
Shetani akuhadaa, kuona bora dunia,
Sasa wamtumikia, pasina kujitambua,
Serikali ilokuwa, Mola inamkataa,
Mtu mwema kumuiza, huhamia ibilisi !
Shere inamfanzia, aliyeumba dunia,
Wao juu wamekuwa, na uchungi wakataa,
Milango waiachia, ibilisi kujimwaa,
Mtu mwema kumuiza, huhamia ibilisi !
Mtu tunamhofia, Mola tunamchezea?
Subira kaichagua, twasema amefulia ?
Yaja tusiyoyajua, kizazi tualilia,
Mtu mwema kumuiza, huhamia ibilisi !
Ibada twazikimbia, sherehe kuziwania,
Muda ametuachia, tawba kuirejea,
Unguja na Tanzania, huruma ninawaonea,
Mtu mwema kumuiza, huhamia ibilisi !
Kitabu twakitania, na dini kuifukia ?
Kati yetu sijajua, nani alokuwa juha,
Ya miezi twaridhia, ya karne twaachia?
Mtu mwema kumuiza, huhamia ibilisi !
JIPENDELEE
NI kama soko dunia, huwezi vyote nunua,
Nawe unapojaliwa, kapu umelichukua,
Utakacho kuchukua, pengine kitakufaa,
Jipendelee mwenzangu, je, kutesa si kwa zamu?
Na unachokujakuwa, mimi siwezi nikawa,
Njia tunazopitia, kamwe sawa hazitakuwa,
Na nitapopumzikia, wewe hautapajua,
Jipendelee mwenzangu, je, kutesa si kwa zamu?
Njiani tullikutania, ndipo tulipoishia,
Itabaki kusikia, pengine kujionea,
Ila pamoja kukaa, tena haitatokea,
Jipendelee mwenzangu, je, kutesa si kwa zamu?
Pamoja tulipokaa, na furaha kuijua,
Fursa tukatumia, nafsi kuziridhia,
Simulizi hubakia, hadi kujiondokea,
Jipendelee mwenzangu, je, kutesa si kwa zamu?
Pendo tuliloadhia, ukaribu ulizua,
Kweli tukaidhania, kumbe ashiki zakoa,
Sura zilipopotea, hamu zikajifia,
Jipendelee mwenzangu, je, kutesa si kwa zamu?
Na hiyo ndiyo dunia, mambo inayoyazua,
katikati hujifia, kustawi haitakuwa,
Unabakia umbeya, na mengi ya kusikia,
Jipendelee mwenzangu, je, kutesa si kwa zamu?
MWENYEZI MUNGU HASHINDWI
WALE wanaodhania, eti Mungu kafulia,
Wangejirudi tabia, subira wakatumia,
Yake keshajipangia, vipi unampangia?
Twapishana kwa wakati, Mwenyezi Mungu hashindwi!
Sivyo anavyoamua, kwa unavyofikiria,
Haendi kwa hatua, unazomhesabia,
Kumi ukijipangia, yeye elfu hutimia,
Twapishana kwa wakati, Mwenyezi Mungu hashindwi!
Subira jina kapewa, mcheleweshaji dunia,
Hatraka akimua, huibadili dunia,
Vikwazo akivitoa, na urahisi kwingia,
Twapishana kwa wakati, Mwenyezi Mungu hashindwi!
PIa aweza amua, ugumu ukaingia,
Kila mnalolifungua, ikawa linakataa,
Hata girisi kitia, bawaba hung'ang'ania,
Twapishana kwa wakati, Mwenyezi Mungu hashindwi!
Majinuni huugua, kweli wakaikataa,
Imani huwaishia, ukafiri kurejea,
Wakawa si wa kusikia, hadi kiyama kwingia,
Twapishana kwa wakati, Mwenyezi Mungu hashindwi!
Mola unayetujua, tasihirili twlailia,
Mioyo kuiridhia, kubuli ikshaingia,
Vingine kutoshania, ili tu kukutegema,
Twapishana kwa wakati, Mwenyezi Mungu hashindwi!
Wangejirudi tabia, subira wakatumia,
Yake keshajipangia, vipi unampangia?
Twapishana kwa wakati, Mwenyezi Mungu hashindwi!
Sivyo anavyoamua, kwa unavyofikiria,
Haendi kwa hatua, unazomhesabia,
Kumi ukijipangia, yeye elfu hutimia,
Twapishana kwa wakati, Mwenyezi Mungu hashindwi!
Subira jina kapewa, mcheleweshaji dunia,
Hatraka akimua, huibadili dunia,
Vikwazo akivitoa, na urahisi kwingia,
Twapishana kwa wakati, Mwenyezi Mungu hashindwi!
PIa aweza amua, ugumu ukaingia,
Kila mnalolifungua, ikawa linakataa,
Hata girisi kitia, bawaba hung'ang'ania,
Twapishana kwa wakati, Mwenyezi Mungu hashindwi!
Majinuni huugua, kweli wakaikataa,
Imani huwaishia, ukafiri kurejea,
Wakawa si wa kusikia, hadi kiyama kwingia,
Twapishana kwa wakati, Mwenyezi Mungu hashindwi!
Mola unayetujua, tasihirili twlailia,
Mioyo kuiridhia, kubuli ikshaingia,
Vingine kutoshania, ili tu kukutegema,
Twapishana kwa wakati, Mwenyezi Mungu hashindwi!
AFAAYE UONGOZI
Sio mtu wa sanaa, wala wa kuionesha,
Ni mja wa kujitambua, mengi anayeng'amua,
Na uchamungu ajua, tawba akaililia,
Afaaye uongozi, dhima huwa akimbia!
Ukubwa atahofia, asije akakosea,
Dhamanaye aijua, ya akhera na dunia,
Humuogopa Jalia, asije kumkosoa,
Afaaye uongozi, dhima huwa akimbia!
Ukubwa huuridhia, akishaiona njia,
Fakiri kusaidia, na zaka kuichangia,
Yawe yanayowafikia, wale waliokusudiwa,
Afaaye uongozi, dhima huwa akimbia!
Ukubwa hautauvaa, kama vile ni kofia,
Watu kumshangilia, na vigelegele kulowa,
Mate akasimbuliwa, na najisi kuchukua,
Afaaye uongozi, dhima huwa akimbia!
Huwa wa kuelekea, ukweli anaoujua,
Hasira kuzihofia, zisije mwangukia,
Kwani ajua dunia, hii ni ya mpito njia,
Afaaye uongozi, dhima huwa akimbia!
Lengo atajiwekea, la hesabu kutimia,
Pasina kitu kupungua, siku itapowadia,
Lulu alizoahidiwa, asije mwingine pewa,
Afaaye uongozi, dhima huwa akimbia!
Kazi anajichapia, ukubwa hatofikiria,
Wenye shida kutatua, wala si kuwanunua,
Uovu akafagia, nchi safi kubakia,
Afaaye uongozi, dhima huwa akimbia!
Zama alikusudiwa, marehemu angekuwa,
Ubaya aliofanyiwa, kwake dawa kuja kuwa,
Mola mwingi wa nazaa, na hadaa azijua,
Afaaye uongozi, dhima huwa akimbia!
Ni mja wa kujitambua, mengi anayeng'amua,
Na uchamungu ajua, tawba akaililia,
Afaaye uongozi, dhima huwa akimbia!
Ukubwa atahofia, asije akakosea,
Dhamanaye aijua, ya akhera na dunia,
Humuogopa Jalia, asije kumkosoa,
Afaaye uongozi, dhima huwa akimbia!
Ukubwa huuridhia, akishaiona njia,
Fakiri kusaidia, na zaka kuichangia,
Yawe yanayowafikia, wale waliokusudiwa,
Afaaye uongozi, dhima huwa akimbia!
Ukubwa hautauvaa, kama vile ni kofia,
Watu kumshangilia, na vigelegele kulowa,
Mate akasimbuliwa, na najisi kuchukua,
Afaaye uongozi, dhima huwa akimbia!
Huwa wa kuelekea, ukweli anaoujua,
Hasira kuzihofia, zisije mwangukia,
Kwani ajua dunia, hii ni ya mpito njia,
Afaaye uongozi, dhima huwa akimbia!
Lengo atajiwekea, la hesabu kutimia,
Pasina kitu kupungua, siku itapowadia,
Lulu alizoahidiwa, asije mwingine pewa,
Afaaye uongozi, dhima huwa akimbia!
Kazi anajichapia, ukubwa hatofikiria,
Wenye shida kutatua, wala si kuwanunua,
Uovu akafagia, nchi safi kubakia,
Afaaye uongozi, dhima huwa akimbia!
Zama alikusudiwa, marehemu angekuwa,
Ubaya aliofanyiwa, kwake dawa kuja kuwa,
Mola mwingi wa nazaa, na hadaa azijua,
Afaaye uongozi, dhima huwa akimbia!
CHA BURE KINGINE GHALI
Humuachia amali, ajuaye jipangia,
Fahari kuwa fahali, dongo lililoumbwa,
Akasema kwa mithali, mjinga hujibomoa,
Sasa nimeshatambua, rahisi nyingine ghali !
Rahisi nyingine ghali, mwanangu nakuambia,
Ikubali idhilali, kidogo kuongezea,
Ukajitoa muhali, ili kesho kukufaa,
Sasa nimeshatambua, rahisi nyingine ghali !
Mbishi hatokubali, bei atapigania,
Kwa kutojua ukweli, aali akakosea,
Muuza akijakubali, thamani keshapangua,
Sasa nimeshatambua, rahisi nyingine ghali !
Huzigundua dalili, haki hatoiridhia,
Kwa kuondoa idhilali, yeye huyakubalia,
Kwisha kuwa kulhali, maisha yakaendelea,
Sasa nimeshatambua, rahisi nyingine ghali !
Haambiliki anzali, huna la kumuelezea,
Hudhani astahili, daima ni kusifiwa,
Akakataa kubuli, na hadaa kununua,
Sasa nimeshatambua, rahisi nyingine ghali !
Humuachia amali, ajuaye jipangia,
Fahari kuwa fahali, dongo lililoumbwa,
Akasema kwa mithali, mjinga hujibomoa,
Sasa nimeshatambua, rahisi nyingine ghali !
MWENYYE THAMANI
Wengine wa kutumiwa, kwa azijuazo ndia,
Kwa ndogo na kubwa gia,yeye keshajipangia,
Yote keshakadiria, thamani kajipangia,
Kila mtaka ukubwa, mwenye thamani ni yeye!
Kiasi anakijua, kaishawahesabia,
Wagawaji kachagua, vibaba kwenda vitoa,
Kikubwa kinachobakia, kuwadi watapatiwa,
Kila mtaka ukubwa, mwenye thamani ni yeye!
Kama shehe anajua, firdausi katwaa,
Kasri keshajipangia, huko aenda ingia,
Bawabu watamjua, wakati keshaingia,
Kila mtaka ukubwa, mwenye thamani ni yeye!
Mbawa atajiotea, na mbinguni akapaa,
Akaicheka dunia, ubora alishajaliwa,
Daraja akatumia, ya kwake kuyaamua,
Kila mtaka ukubwa, mwenye thamani ni yeye!
Huiba akafidia, kule kulikopungua,
Asopendwa huonewa, kidogo kutoachiwa,
Mbavu wakazikazia, dhiki kumshambulia,
Kila mtaka ukubwa, mwenye thamani ni yeye!
Ila wanaomsifia, karamu watafanziwa,
Vitu kuteremshiwa, hata wasivyofikiria,
Ipambwe yao dunia, mauti kuyatania,
Kila mtaka ukubwa, mwenye thamani ni yeye!
FISADI AKISHAANZA
Nani amekwambia, eti kushiba ajua,
Huyo akishaanzia, daima huwa na njaa,
Tumbo huzidi panua, kama Jetwa hujakua,
Fisadi akishaanza, huwa haachi fasidi!
Fisadi mwana balaa, haramu hatokimbia,
Hutaka kuongezewa, hadi mapipa kujaa,
Raha akajionea, eti kwa k uangalia,
Fisadi akishaanza, huwa haachi fasidi!
Wa ndani humuibia, pasipo ya kutambua,
Cha nje kinapokuwa, kwa deni aweza ua,
Moja ataikimbilia, mia akaziachia,
Fisadi akishaanza, huwa haachi fasidi!
Nikahi anayoijua, ya nje ikitokea,
Kifua huikingia, wa ndani wakaasiwa,
Mitupu waliyokuwa, nani atajilambia?
Fisadi akishaanza, huwa haachi fasidi!
Fisadi mwana tamaa, na sifa huziogea,
Daima huzililia, jasmini yakatiwa,
Udi na uvumba pia, Uarabu kujitia,
Fisadi akishaanza, huwa haachi fasidi!
Hujaribu mwanakuwa, kuikusanya dunia,
Akashindwa kutambuwa, yeye ndiye atakiwa,
Kukusanywa na kutiwa, kwenye la sahau jaa,
Fisadi akishaanza, huwa haachi fasidi!
Mola atampangia, nini ataka fanyiwa,
Na siku kujiwekea, hakika akaitia,
Pasina kujitambua, nyuzi zilizobakia,
Fisadi akishaanza, huwa haachi fasidi!
Ya Afu nakuangukia, karama kunigawia,
La kesho wasilojua, miye nikalitambua,
Mbali nao nikakaa, na kuistadi dunia,
Fisadi akishaanza, huwa haachi fasidi!
HASARA KUBWA KWA N CHI
Rahisi kununuliwa, mfukoni akatiwa,
Kisha akajatumiwa, mwenyewe kuja jiua,
Hajui anachojua, msukule keshakuwa,
Hasara kubwa kwa nchi, kijana asojijua !
Atafuta ganga njaa, sio kiongozi kuwa,
Dhiki akaiondoa, katikati amekaa,
Wabaya kuwaondoa, watu wanaonunua,
Hasara kubwa kwa nchi, kijana asojijua !
Kujiamini silaha, yeye asiyochukua,
Kubebwa keshazoea, kila kitu hufanziwa,
Kutafuta hatajoua, sikuzote wa kupewa,
Hasara kubwa kwa nchi, kijana asojijua !
Huiabudu dunia, Mola akamkimbia,
Upepo akishatiwa, akazidi kuvimbiwa,
Hadi juu hujaa, kwenye anga akapaa,
Hasara kubwa kwa nchi, kijana asojijua !
Hapo anapofiikia, Mungu huja jidhania,
Wahyi akautoa, kwa amri zisokuwa,
Hajui la kutumiwa, wala la kufikiria,
Hasara kubwa kwa nchi, kijana asojijua !
Kiatu husiginia, watakaomsaidia,
Akili akadhania, pekee amejaliwa,
Kumbe hajajijua, kubaya aogelea,
Hasara kubwa kwa nchi, kijana asojijua !
MWENYE KUTOA KWA DHATI
HATAKI kuangaziwa, sadaka akiitoa,
Kwenye siri huingia, Molawe kumuachia,
Viumbe kutotegemea, kitu kumsaidia,l
Mwenye kutoa kwa dhati, tivii huiogopa!
Uungu huukimbia, na riziki kuzigawa,
Apendwaye akapaewa, asopendwa kuchukiwa,
Riziki akakatiwa, na matatani kutiwa,
Mwenye kutoa kwa dhati, gazeti huliogopa!
Mola humtangulia, afaaye ogopewa,
Ndiyo wa kutetemekewa, milki anayegawa,
Na ukuu kuwagiwa, wale anaochagua,
Mwenye kutoa kwa dhati, inteneti huogopa!
Mitihani aijua, kunaguka huhofia,
Asije kuteketea, badala kujiokoa,
Waliomtangulia, zao keshaelezewa,
Mwenye kutoa kwa dhati, redio huzikimbia!
Nafsi aitambua, ilivyojaa hadaa,
Uungu ikalilia, japo kifo chaingojea,
Ila uhai ukiwa, kila kitu hugombania,
Mwenye kutoa kwa dhati, tivii huiogopa!
Kazi moja aijua, mbingu zinaiongojea,
Ibada ya kutulia, na kisha kusaidia,
Kwa faragha kuamua, na kutenda vivyo pia,
Mwenye kutoa kwa dhati, gazeti huliogopa!
Hatonjojea mataa, na kamera kuletwa,
Dunia ipate mjua, ni nani aliyetoa,
Kwani anatambua, walipaji hawajawa,
Mwenye kutoa kwa dhati, inteneti huogopa!
Mlipaji katulia, yeye ajitazamia,
Malaika wahadithia, viumbe zao tabia,
Taarifa huletewa, wa kweli wakawajua,
Mwenye kutoa kwa dhati, redio huzikimbia!
mtu asiyejijua
Vyovyote anatumiwa, na wengine
kuwafaa,
Yeye kama chombo huwa, mashinani
kusagiwa,
Mtu kutojitambua, utumwa kwake
tabia!
Hushindwa 'jifikiria, sembuse
kufikiria?
Kama vile ndoo kuwa, au karai
kutumiwa,
Zege akalichangia, pasina na sifa
kuwa,
Mtu kutojitambua, utumwa kwake
tabia!
Dezo atanunuliwa, na walionunuliwa,
Mfukoni akatiwa, ndivyo sivyo
kutumiwa,
Vishilingi akipewa, tajiri
akajisikia,
Mtu kutojitambua, utumwa kwake
tabia!
Kwa cheo huzainiwa, hata wana
kuwaua,
Ukuu akauwania, kwa damu kujimwagia,
Hesabu akijaijua, hubaki kujijutia,
Mtu kutojitambua, utumwa kwake
tabia!
Mara huchanganyikiwa, misuli
kuitanua,
Kisha akaazimia, kuikusanya dunia,
Hajui hatobakia, dunia kumngojea,
Mtu kutojitambua, utumwa kwake
tabia!
Miaka keshahesabia, kisha motoni
kwingia,
Milele kwenda kukaa, kwa anayoyamua,
Laiti angetambua, vivyo asingetumiwa,
Mtu kutojitambua, utumwa kwake
tabia!
Roho inapotolewa, ndio ukweli hujua,
Tena sana akalia, dakika kuruhusiwa,
Mema akachangia, moto kwenda
ukimbia,
Mtu kutojitambua, utumwa kwake
tabia!
Rushwa hutaka kutoa, malaika kugawia,
Wapate kumuachia, dakika akasalia,
Ila hatohurumiwa, macho akayakodoa,
Mtu kutojitambua, utumwa kwake
tabia!
Huwezi kuwazaini
KUWA bingwa wa hadaa, na kofia
kuzivaa,
Kamwe hautojaliwa, wote wakakusikia,
Lako kulihudumia, ukweli ukauawa,
Huwezi kuwazaini, watu wote, pande
zote!
Idadi hutachukua, ya bure na
kununua,
Ndicho tulichoumbiwa, viumbe
tuliopotea,
Utumwani hujitia, wenyewe kwa
kuchagua,
Huwezi kuwazaini, watu wote, rika
zote!
Kamba huwa ni hidaya, mkononi
kuzitia,
Kisha kujitundukia, tunapoamriwa,
Amri kuzisikia, hata zilizo ukiwa,
Huwezi kuwazaini, watu wote, siku
zote!
Hatuwi wa kuchagua, ya kwetu
kufikiria,
Kubebwa tumezoea, hatutaki kutembea,
Kiyama kinatujia, hali twakiangalia,
Huwezi kuwazaini, watu wote, pande
zote!
Twashindwa kuyaamua, ya kwenda
kutuokoa,
Firdausi kuingia, pepo ya kuteuliwa,
Mithili isiyokuwa, wala haitatokea,
Huwezi kuwazaini, watu wote, rika
zote!
Twashndwa kujichagua, vikongwe
kukimbilia,
Mikongojo sisi kuwa, badala ya
kujisimamia,
Ushauri nautoa, bongo zetu kufungua,
Huwezi kuwazaini, watu wote, siku
zote!
Bongo zetu kufungua, kofuli
kuziondoa,
Funduo kuzitumia, Mola keshatupatia,
Njia mkishahofia, mbele kutoendelea,
Huwezi kuwazaini, watu wote, pande
zote!
Msije kuyayatuia, kwamba haya
mliambiwa,
Nanyi hamkusikia, dhihaka mkaitia,
Wa kweli anayejua, pande hatoegemea,
Huwezi kuwazaini, watu wote, rika
zote!
Rabuka namsifia, itihari kujaliwa,
Kweli nikapigania, na haki
kuigombea,
Japo fakiri nikiwa, ikawa yangu
ridhaa,
Huwezi kuwazaini, watu wote, siku
zote!
Subscribe to:
Posts (Atom)