WALE wanaodhania, eti Mungu kafulia,
Wangejirudi tabia, subira wakatumia,
Yake keshajipangia, vipi unampangia?
Twapishana kwa wakati, Mwenyezi Mungu hashindwi!
Sivyo anavyoamua, kwa unavyofikiria,
Haendi kwa hatua, unazomhesabia,
Kumi ukijipangia, yeye elfu hutimia,
Twapishana kwa wakati, Mwenyezi Mungu hashindwi!
Subira jina kapewa, mcheleweshaji dunia,
Hatraka akimua, huibadili dunia,
Vikwazo akivitoa, na urahisi kwingia,
Twapishana kwa wakati, Mwenyezi Mungu hashindwi!
PIa aweza amua, ugumu ukaingia,
Kila mnalolifungua, ikawa linakataa,
Hata girisi kitia, bawaba hung'ang'ania,
Twapishana kwa wakati, Mwenyezi Mungu hashindwi!
Majinuni huugua, kweli wakaikataa,
Imani huwaishia, ukafiri kurejea,
Wakawa si wa kusikia, hadi kiyama kwingia,
Twapishana kwa wakati, Mwenyezi Mungu hashindwi!
Mola unayetujua, tasihirili twlailia,
Mioyo kuiridhia, kubuli ikshaingia,
Vingine kutoshania, ili tu kukutegema,
Twapishana kwa wakati, Mwenyezi Mungu hashindwi!
Monday, August 26, 2013
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
No comments:
Post a Comment