KUWA bingwa wa hadaa, na kofia
kuzivaa,
Kamwe hautojaliwa, wote wakakusikia,
Lako kulihudumia, ukweli ukauawa,
Huwezi kuwazaini, watu wote, pande
zote!
Idadi hutachukua, ya bure na
kununua,
Ndicho tulichoumbiwa, viumbe
tuliopotea,
Utumwani hujitia, wenyewe kwa
kuchagua,
Huwezi kuwazaini, watu wote, rika
zote!
Kamba huwa ni hidaya, mkononi
kuzitia,
Kisha kujitundukia, tunapoamriwa,
Amri kuzisikia, hata zilizo ukiwa,
Huwezi kuwazaini, watu wote, siku
zote!
Hatuwi wa kuchagua, ya kwetu
kufikiria,
Kubebwa tumezoea, hatutaki kutembea,
Kiyama kinatujia, hali twakiangalia,
Huwezi kuwazaini, watu wote, pande
zote!
Twashindwa kuyaamua, ya kwenda
kutuokoa,
Firdausi kuingia, pepo ya kuteuliwa,
Mithili isiyokuwa, wala haitatokea,
Huwezi kuwazaini, watu wote, rika
zote!
Twashndwa kujichagua, vikongwe
kukimbilia,
Mikongojo sisi kuwa, badala ya
kujisimamia,
Ushauri nautoa, bongo zetu kufungua,
Huwezi kuwazaini, watu wote, siku
zote!
Bongo zetu kufungua, kofuli
kuziondoa,
Funduo kuzitumia, Mola keshatupatia,
Njia mkishahofia, mbele kutoendelea,
Huwezi kuwazaini, watu wote, pande
zote!
Msije kuyayatuia, kwamba haya
mliambiwa,
Nanyi hamkusikia, dhihaka mkaitia,
Wa kweli anayejua, pande hatoegemea,
Huwezi kuwazaini, watu wote, rika
zote!
Rabuka namsifia, itihari kujaliwa,
Kweli nikapigania, na haki
kuigombea,
Japo fakiri nikiwa, ikawa yangu
ridhaa,
Huwezi kuwazaini, watu wote, siku
zote!
No comments:
Post a Comment