Shetani keshajitoma, ndaniyo ametulia,
Dhamiri tokea zama, yako kkutibulia,
Ukaikimbia njia, ya uzima pia twaha,
Mtu mwema kumuiza, huhamia ibilisi !
Shetani akuhadaa, kuona bora dunia,
Sasa wamtumikia, pasina kujitambua,
Serikali ilokuwa, Mola inamkataa,
Mtu mwema kumuiza, huhamia ibilisi !
Shere inamfanzia, aliyeumba dunia,
Wao juu wamekuwa, na uchungi wakataa,
Milango waiachia, ibilisi kujimwaa,
Mtu mwema kumuiza, huhamia ibilisi !
Mtu tunamhofia, Mola tunamchezea?
Subira kaichagua, twasema amefulia ?
Yaja tusiyoyajua, kizazi tualilia,
Mtu mwema kumuiza, huhamia ibilisi !
Ibada twazikimbia, sherehe kuziwania,
Muda ametuachia, tawba kuirejea,
Unguja na Tanzania, huruma ninawaonea,
Mtu mwema kumuiza, huhamia ibilisi !
Kitabu twakitania, na dini kuifukia ?
Kati yetu sijajua, nani alokuwa juha,
Ya miezi twaridhia, ya karne twaachia?
Mtu mwema kumuiza, huhamia ibilisi !
Monday, August 26, 2013
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
No comments:
Post a Comment