Walio na njaa huwa, chakula wakimbilia,
Kukila tumbo kujaa, na maji wakajazia,
Wala sio kuchezea, mchanga wakakitia,
Wapo wenye nja'ya kula, na njaa ya kuharibu!
Wenye ya ajabu njaa, israfu wanatia,
Chakula hukichezea, kwani si ya kweli njaa,
Sana walikililia, ili sheri kufanzia,
Wapo wenye nja'ya kula, na njaa ya kuharibu!
Matumbo yamewajaa, wazito utadhania,
Bado wakakililia, hali kuishatkia,
Pindi wanapopatiwa, huanza kukichezea,
Wapo wenye nja'ya kula, na njaa ya kuharibu!
No comments:
Post a Comment