Thursday, December 13, 2012

M K U B W A


Kazi nimejifanzia, wajibu iliyokuwa,
Cheo nilishakipewa, ziada naikataa,
Hapa nilipofikia ukubwa kwangu hadaa,
Lipi nililolifanza, hata niitwe mkubwa!

Ukubwa kwangu hadaa, ziada isiyofaa,
Na anayenyenyekea, h ofu sana anitia,
Yuleyule nilikuwa, yuleyule nitakuwa,
Lipi nililolifanza, hata niitwe mkubwa!

No comments: