Kazi nimejifanzia, wajibu iliyokuwa,
Cheo nilishakipewa, ziada naikataa,
Hapa nilipofikia ukubwa kwangu hadaa,
Lipi nililolifanza, hata niitwe mkubwa!
Ukubwa kwangu hadaa, ziada isiyofaa,
Na anayenyenyekea, h ofu sana anitia,
Yuleyule nilikuwa, yuleyule nitakuwa,
Lipi nililolifanza, hata niitwe mkubwa!
No comments:
Post a Comment