UCHAMA naukataa, haki nazingatia,
Ni mwana demokrasia, pembeni aliyekaa,
Haki kuilingania, itulie mizania,
Si mshairi wa chama, na wala haitakuwa !
Nateta demokrasia, izagae Tanzania,
Udikteta uchwara, chembe kutobakia,
Yale ya chama kimoya, yatoke yasiyofaa,
Si mshairi wa chama, na wala haitakuwa !
Usawa naupigania, fakiri kusaidia,
Vijijii wlaiokuwa, huko kusikoangaliwa,
Hali juu kuinua, makwao kujivunia,
Si mshairi wa chama, na wala haitakuwa !
Ukinitaka ubia, na wew weza ingia,
Vijijini kuingia, ya kwao tukayanoa,
Bongo tukiwapatia, kufikiri wanajua,
Si mshairi wa chama, na wala haitakuwa !
Mipango ukiandaa, kusoma wanaelewa,
Mita ukiwaambia, ni kipimo wakijua,
Umbali ukiongea, wnaaweza kufikia,
Si mshairi wa chama, na wala haitakuwa !
Wazo ukilichimbua, lulu wataigundua,
Haba na haba ikawa, mbele weza endelea,
Mzawa asipojifaa, hivi nani kumfaa?
Si mshairi wa chama, na wala haitakuwa !
No comments:
Post a Comment