AJABU
itatokea, wewe uliyefuatia,
Kidomo
ukajitia, kwa alotangulia,
Uapizo
kuutia, eti kwani wachukia,
Aliyekutangulia,
waweza kumuapiza ?
Kama
panao ubaya, mukubuli huwa dua,
Ila
onyo ukipewa, watakiwa lichukua,
Vingine
ukiamua, madhila unajitia,
Aliyekutangulia,
waweza kumuapiza ?
Leo
hutofikiria, hadi kesho ikiingia,
Ikawa
umechelewa, yakufika yametua,
Na
hii ndiyo dunia, ilivyo yake tabia,
Aliyekutangulia,
waweza kumuapiza ?
Subira
ukiijua, neno utalifatia,
Kisha
ukalichimbua, na mizizi kuing'oa,
Kama
mhogo kuliwa, na sumu kuondolewa,
Aliyekutangulia,
waweza kumuapiza ?
Pepo
katika dunia, huwa zina ya kuzua,
Hasa
zikakurubia, tanga kwenda zisumbua,
Na
vyombo vikaelea, kule visikotakiwa,
Aliyekutangulia,
waweza kumuapiza ?
Wengi
yamewazuzua, bora wakayaachia,
Haraka
kukimbilia, ziliokofika tamaa,
Wakija
kujigundua, wakabakia kulia,
Aliyekutangulia,
waweza kumuapiza ?
Vibaka
kwenye dunia, daraja walishapewa,
Wa
chini hutuhunia, wa juu twawachukua,
Pasina
sisi kujua, mijitumwa kubakia,
Aliyekutangulia,
waweza kumuapiza ?
Yao
yakatengamaa, na yetu tukafulia,
Na
saa ikiwadia, litafunguka pazia,
Nje
tukajionea, sivyo ilivyotakiwa,
Aliyekutangulia,
waweza kumuapiza ?
No comments:
Post a Comment