KAMA
mbuyu na mkuyu, tambiko lilipokaa,
Watu
huja kwa miguu, kuja soma zao dua,
Kafara
wasisahau, mashinani kuzitoa,
Tambiko
likiondoka, koo husambaratika !
Wazazi
huyanukuu, mila zikafuatia,
Wakarithi
wajukuu, na kizazi kwendelea,
Kwa
gharama na nafuu, hakuna wa kuchimbua,
Tambiko
likiondoka, koo husambaratika !
Wazima
nao mafuu, kuuuliza hukataa,
Wakahofu
ubahau, kizazi kutunukiwa,
Au
ya koo dharau, na wengine kuchukia,
Tambiko
likiondoka, koo husambaratika !
Lilipo
ni sikukuu, hadi likijang'olewa,
Pakabaki
kichuguu, mchwa kwenda kuhamia,
Yakaanza
mahuruhu, makaburi kufagia,
Tambiko
likiondoka, koo husambaratika !
Moyo
wangu ni juzuu, hapa nilipofikia,
Hakijaja
kitukuu, na sijaijua dunia,
Na
sijda na rukuu, wala hazijatimia,
Tambiko
likiondoka, koo husambaratika !
Si
cha maji kitunguu, na saumu sijakuwa,
Nazihofu
dafrau, za siasa na kuzua,
Naitafuta
nafuu, penye ukiwa kukaa,
Tambiko
likiondoka, koo husambaratika !
Nawaachia
ukuu, waliobeba dunia,
Mimi
naenda sahau, yote nikayaachia,
Nikahifadhi
nahau, wajukuu kuzijua,
Tambiko
likiondoka, koo husambaratika !
Namshukuru
Afuu, hapo nilipofikia,
Mukubuli
nanukuu, yake nimeyaridhia,
Naendeleza
juzuu, daraja nende patiwa,
Tambiko
likiondoka, koo husambaratika !
No comments:
Post a Comment