KAMA hujaligundua, wala siri
haijawa,
Kwa tunakoelekea, uhuni
wafichuliwa,
Dhahiri inaingia, watu wote
kuijua,
Umoja wa kitaifa, ni vigumu
kukwepeka!
Ukabila Tanzania, wa chama
umebakia,
Na nchi kuiokoa, ni lazima
kujifia,
Usawa ukaingia, nafasi kupigania,
Umoja wa kitaifa, ni vigumu
kukwepeka!
Koo tutajazigawa, uchama
kuendelea,
Na vijiji kufulia, kitu visije
ambua,
Uongo tunaozua, haujengi,
wabomoa,
Umoja wa kitaifa, ni vigumu
kukwepeka!
IJe mbele Tanzania, mengine
yakafatia,
Vinginevyo tutalia, nchi
tukaililia,
Tanzania, Tanzania, nchi yangu
wapotea,
Umoja wa kitaifa, ni vigumu
kukwepeka!
Wote tunajitambua, uhai unatufaa,
Wazushi wa kuzuzua, lazima
kuwafichua,
Mkao wanaokaa, haunao njema nia,
Umoja wa kitaifa, ni vigumu
kukwepeka!
Wengine wanahofiwa, shetani
awatumia,
Kichwani keshaingia, mbio
awafukuzia,
Ya shari kukimbilia, nchi ije
angamia,
Umoja wa kitaifa, ni vigumu kukwepeka!
Nusura tukiijua, vyema
tutawachingua,
Sababu na yao nia, ukubwa
kuulilia,
Au ikulu inshakuwa, danguro la
kuhamia?
Umoja wa kitaifa, ni vigumu
kukwepeka!
Waliojaa madoa, na hata likiwa
doa,
Ushauri nautoa, ngazi budi
kuachia,
Safi tunaodhania, gidamu
wakachukua,
Umoja wa kitaifa, ni vigumu
kukwepeka!
Haiwi haitakuwa, ubora wa
kununua,
Halali ukajitia, na ngazi
kujipandia,
Hima haitasalia, nia itakubetua,
Umoja wa kitaifa, ni vigumu
kukwepeka!
Mapema naashiria, siri
zinafichuliwa,
Mengi tusiyoyajua, mbona sasa
twayajua,
Kila mwanzia ubaya, hatima huwa
ubaya,
Umoja wa kitaifa, ni vigumu
kukwepeka!
Vyama vyetu hujifia, hoja
zinapopungua,
Na uchafu kununua, wengine
kuwatupia,
Hadhari ninaitoa, hiyo kwetu siyo
njia,
Umoja wa kitaifa, ni vigumu
kukwepeka!
Wanasiasa mwafaa, kuikoa Tanzania,
Nafasi mkiachia, mtakuja
kuzomewa,
Umoja mngeanzia, wa vyama
kupigania,
Umoja wa kitaifa, ni vigumu
kukwepeka!
Kisha mkajichungua, bora wenu
kuwajua,
Bila ya kufikiria, chama gani
atokea,
Nahodha anayefaa, nchi hii
kuokoa,
Umoja wa kitaifa, ni vigumu
kukwepeka!
Mipaka mkaondoa, kwa adili
kuijua,
Na safi kilichokuwa, nchi
mkaipatia,
Imani zinatakiwa, kazi hii
kutetea,
Umoja wa kitaifa, ni vigumu
kukwepeka!
Twataka atayetufaa, na wala sio
balaa,
Tunataka manufaa, wala si
kuhofia,
Salama ya Tanzania, alo bora
kuchagua,
Umoja wa kitaifa, ni vigumu
kukwepeka!
No comments:
Post a Comment