Ndivyo
ilivyo dunia, watu huipigania,
Na
wanachopigania, hamu ikawaishia,
Wakishakujipatia,
tafrani zikapoa,
Wewe
ukishakipata, changamoto hupotea!
Husumbuka
na dunia, bilkuli kuwania,
Kwa
linalowazuzua, mfukoni kulitia,
Hamadi
likitulia, ari inadidimia,
Wewe
ukishakipata, changamoto hupotea!
Mbio
watazitimua, nyikani wakapotea,
Marathoni
mara kuwa, ovyo wanajihemea,
Ila
wakiambulia, hurudi wakatulia,
Wewe
ukishakipata, changamoto hupotea!
Hutamani
ya dunia, na wao kujipatia,
Mikononi
wakitia, hawa inawaishia,
Jingine
kuangalia,wapi la kulifuatia,
Wewe
ukishakipata, changamoto hupotea!
Hutetemesha
jamaa, hadi wakamchukia,
Na
dharau kuzitoa, vishindo akavitia,
Akatingisha
dunia, tunda kwenda liangua,
Wewe
ukishakipata, changamoto hupotea!
Likija
mdondokea, kudaka huparamia,
Kisha
akachuchumia, mikononi kulitia,
Anapoliangalia,
si dhahabu akajua,
Wewe
ukishakipata, changamoto hupotea!
No comments:
Post a Comment