Ninaianza tasua, kwa pazia
kulitoa,
Jalali kaniridhia, shukrani
ninatoa,
Siye niliyeanzia, karne
zimeshatimia,
Dua zetu huwa dawa, uchamungu
ukiwepo!
Viumbe hujifutua, uovu kuparamia,
Kama mipira ikawa, kudunda
watarajia,
Ya watu huwazuzua, pabaya
wakaingia,
Dua zetu huwa dawa, uchamungu
ukiwepo!
Chini wanapoanzia, hudhania ni
wakiwa,
Juu wakishafikia, pumzi
huzitanua,
Fahari wakatamia, na kiburi
kukitia,
Dua zetu huwa dawa, uchamungu
ukiwepo!
Ujibari ukakua, ya Mola
kuyachezea,
Visa mkasa ikawa, kwao ndio
mazoea,
Ila siku hufikia, ukweli
wakaujua,
Dua zetu huwa dawa, uchamungu
ukiwepo!
Ila siku hufikia, ukweli
wakaujua,
Hasa wanapoingia, imani
iliyowakaa,
Mukubuli yao kuwa, yasiache
kupokewa,
Dua zetu huwa dawa, uchamungu
ukiwepo!
Uchamungu ukitua, meseji
haitapotea,
Wenda inapotakiwa, kwa wakati
kuingia,
Ikajionea dunia, ujumbe wakaujua,
Dua zetu huwa dawa, uchamungu
ukiwepo!
Majina yetu bandia, kwa mengi
sana twapwaya,
Vitabu twaviambaa, na dua
kutozijua,
Nazo ibada kadhaa, zingine
zinapotea,
Dua zetu huwa dawa, uchamungu
ukiwepo!
Wakati umewadia, Yarabi
kumrejelea,
yake tukasimamia, na hali njema
ikawa,
Pamwe naye tutakuwa, bishara
tukizitoa,
Dua zetu huwa dawa, uchamungu
ukiwepo!
Nyakati zajifungua, sana wazi
zinakuwa,
Gizani tuliyokuwa, mwanga sasa
waingia,
Efemu kiifungua, chuoni unaingia,
Dua zetu huwa dawa, uchamungu
ukiwepo!
Daraja unayetoa, hadh yetu
angalia,
Shere wanaokusudia, mkengeni
kuwatia,
Kamba umetupatia, tuwezeshe kutumia,
Dua zetu huwa dawa, uchamungu
ukiwepo!
No comments:
Post a Comment