Mola anayemridhia, hakosi kumgutua,
Kisa kinapotokea, akawa mwenye
kujua,
Toba inayongojewa, si ile ya
kutania,
Mtu akistuliwa, haachi kujitambua
!
Hadharani hutokea, pasina kawa
kutiwa,
Watu wakajionea, na ishara
kuijua,
Yapo ya kuyachezea, mengine ni
kujiua,
Mtu akistuliwa, haachi kujitambua
!
Maumbile huacha, kazi
yakajifanzia,
Vifua ikakunjua, hisia kuzielewa,
Kila asiyelaaniwa, tanzu
akazitambua,
Mtu akistuliwa, haachi kujitambua
!
Katika hii dunia, michache
inabakia,
Anayejielewa, ajua la kuamua,
Anayezuzuliwa, hubakia kuchezea,
Mtu akistuliwa, haachi kujitambua
!
Kinyago huchukuliwa, hadhiye
anayopewa,
Mola akampatia, kambaye
kuning'inia,
Akija kushtukia, wasaa
unshawadia,
Mtu akistuliwa, haachi kujitambua
!
Vidole huvitanua, alama akavitia,
Kisha vikakunjuliwa, ufahamu
kuutia,
Kula mwenye kujaliwa, adhana
akasikia,
Mtu akistuliwa, haachi kujitambua
!
Kazi tunazojipea, daraja
zinapungua,
Ila kwa kutokujua, bora
tunazidhania,
Shetani akatuvaa, tukashindwa
kuachia,
Mtu akistuliwa, haachi kujitambua
!
Shehe Ali alijua, aweza
kusimulia,
Baraza wakaikaa, na hali
kuangalia,
Vingine vinavyotokea, vyawasuta
wasokuwa,
Mtu akistuliwa, haachi kujitambua
!
Namshukuru Jalia, fikra
kunijalia,
Kuwaza na kuwazua, na wengine
kumegea,
Uchoyo sikujaliwa, japo tajiri
sijawa,
Mtu akistuliwa, haachi kujitambua
!
No comments:
Post a Comment