Hainitezi
dunia, yake nikakimbilia,
Ni
kiboko wa hadaa, ilipo huifichua,
Ujinga
hatukuzawa, na kwao hatukuumbiwa,
Hadaa
naikataa, hiyo ndiyo siri yangu !
Siku
unakaribia, mafuta kujiondoa,
Juu
kuja kuelewa, maji chini kubakia,
Kweli
itapoingia, na uongo kujitoa,
Uongo
katu sipendi, hiyo ndiyo siri yangu!
Siku
inakaribia, mjinga kujielwa,
Werevu
ukazaliwa, na hoja zikatolewa,
Wajanja
wasiojua, aibu kuwaingia,
Umbeya
naukimbia, hiyo ndiyo siri yangu!
Pia
nao wa kuzua, hesabu wahesabiwa,
Namba
ikishafikia, yote moja itakuwa,
Hapana
la kujaliwa, ni ukweli kurejea,
Shiriki
siikubali, hiyo ndiyo siri yangu!
Na
wanaomswalia, shetani pasi kujua,
Wito
watausikia, roho zikawagutuwa,
Ubaya
wakaujua, na talaka kuitoa,
Wema
hakika ni jadi, hiyo ndiyo siri yangu!
Mitego
wataijua, izukapo adilia,
Ukweli
ikafichua, hekalu kutengemaa,
Shetani
atapolia, na uchi akajijua,
Fitina
huwa sitaki, hiyo ndiyo siri yangu!
Si
nabii wa kuvaa, majoho yasiyokuwa,
Kwa
kuifata hadaa, na vitimbi vya dunia,
Na
utume sikupewa, zama ulikwishaishia,
Maneno
huwa sipendi, hiyo ndiyo siri yangu!
Nilipo
nimetulia, funguo nazingojea,
Ukiingia
wasaa, nije kuwasimulia,
Hakika
wa kurejea, visa hawezi kuzua,
Vitendo
kwangu ashiki, hiyo ndiyo siri yangu!
Nimezitoa
hisia, ujumbe kuwafikia,
Haya
mkifikiria, mema yanawangojea,
Ila
ninachohofia, mtihani kujikomboa,
Kuendeleza
wengine, hiyo ndiyo siri yangu.
Namshukuru
Jalia, kwa dhikiri kuitoa,
Nao
waliojaliwa, langu wamelisikia,
Yawangojea
hatua, daraja kuifikia,
Kuridhika
na kadari, hiyo ndiyo siri yangu!
No comments:
Post a Comment