Dunia
inaegema, mashariki kuhamia,
Ndiko
kuliko neema, na salama kujaliwa,
Mzazi
aliye mwema, mwana atamwambia,
Uchina
kasomesheni, kwa nafuu na salama !
Wanaolea
dhuluma, yawakimbia dunia,
Kwingineko
wamehama, Afrika kuhamia,
Maisha
yao nakama, na watu kuvurugia,
Uchina
kasomesheni, kwa nafuu na salama !
Mchina
awapa homa, hawakai wakakaa,
Wanakiona
kiama, si mbali kinaajia,
Afrika
kuigema, ndiyo kubwa yao nia,
Uchina
kasomesheni, kwa nafuu na salama !
Wamezoea
kuchuma, kwa wengine kuibia,
Maziwa
wanayokama, kutoka yanakataa,
Matumbo
yawanguruma, wapi kwenda kuhamia,
Uchina
kasomesheni, kwa nafuu na salama !
Maisha
yao daima, kwa wengine kwenda vua,
Hawajali
yako hima, nuksi hukuachia,
Wa
kwako wakaroroma, na silaha kuzikwea,
Uchina
kasomesheni, kwa nafuu na salama !
Maisha
yao hujuma, na msaada udhia,
Vipi
wewe mtu mzima, lawalawa wapokea,
Mgodi
ukautema, bakshishi kupokea?
Uchina
kasomesheni, kwa nafuu na salama !
Busara
zimetuhama, ni watu wa kubabia,
Twadharau
wetu umma, wageni watuzuzua,
Kigingi
ni mkulima, mnunuzi hatokaa,
Uchina
kasomesheni, kwa nafuu na salama !
Imepotea
hekima, kwa ukubwa kulilia,
Hapo
tulipoegema, mbona mengi tumepwaya,
Hii
ya ovyo kalima, lazima kuumbuliwa,
Uchina
kasomesheni, kwa nafuu na salama !
Wewe
baba, wewe mama, Zatakiwa njia mpya,
Kituo
cha kusimama, kuanzia Malaysia,
Indonesia
nako hima, panafaa kuchungua,
Uchina
kasomesheni, kwa nafuu na salama !
Za
wazungu ni gharama, sasa zitatuumbua,
Rushwa
kuwa mlima, tushinde kujipandia,
Twendeni
kwenye neema, kwenye njaa kukimbia,
Uchina
kasomesheni, kwa nafuu na salama !
Wakwezi
ninawatuma, wengine kuwaambia,
Hususan
Wakulima,Morogoro walokaa,
Halafu
ninawatuma, wafugaji kuwaambia,
Uchina
kasomesheni, kwa nafuu na salama !
Nchi
yataka neema, na elimu kuenea,
Ikipungua
gharama, wengi tutafanikiwa,
Na
katika hizi zama, ubia unatakiwa,
Uchina
kasomesheni, kwa nafuu na salama !
Ubia
sasa lazima, na vyuo vya Malayasia,
Akili
wakzituma, kuhamia Tanzania,
Na
matawi kuyafuma, urahisi kwetu kuwa,
Uchina
kasomesheni, kwa nafuu na salama !
Ubia
kitu cha hima, na Wachina kuingia,
Vyuo
kwao vikahama, kuhamia Tanzania,
Mitandao
ikafuma, ubora sawa ukawa,
Uchina
kasomesheni, kwa nafuu na salama !
Ninamuomba
Rahima, macho kuja tufungua,
Tukaipata
neema, sana tunayoililia,
Zigeuke
zetu zama, kwa nafuu kuingia,
Uchina
kasomesheni, kwa nafuu na salama !
No comments:
Post a Comment