Isije
sasa ikawa, ndugu umekwishapagawa,
Unataka
kuchezewa, ngoma tusiyoijua,
Na
kibwebwe wajitia, uwanjani kuingia ?
Unataka
kusifiwa, kwa wajibu kutimiza?
Utoto
unatutia, kama tusiotambua,
Kile
unachotakiwa, kwa ngwee kujilimia,
Twaona
inapungua, wewe wzidi tutambia?
Unataka
kusifiwa, kwa wajibu kutimiza?
Sasa
umelichokoa, nasi tunalizomea,
Vigelegele
ikiwa, kama havitasinzia,
Ukweli
watu wajua, vingine haitakuwa,
Unataka
kusifiwa, kwa wajibu kutimiza?
Ni
nani anayejua, mbali tungeshafikia,
Laiti
ingelikuwa, haki imesimamiwa,
Na
fisadi kuwaniwa, masomaso kuwatoa,
Unataka
kusifiwa, kwa wajibu kutimiza?
Tambo
ninazishangaa, kwa kazi za kupangiwa,
Na
saada la kufaa, nyuma limeshehenea,
Kisha
mtu kuwazia, sifa akajipambia,
Unataka
kusifiwa, kwa wajibu kutimiza?
Kiherehere
najua, watu wengi waugua,
Na
tivii kutujia, wote tunakimbilia,
Hata
wenye sura mbaya, wapenda kumulikiwa,
Unataka
kusifiwa, kwa wajibu kutimiza?
Hayo
ninajionea, nashindwa kuvumilia,
Adili
naililia, uongo kuukimbia,
Nchi
haitofanikiwa, mbwembwe tukitegemea,
Unataka
kusifiwa, kwa wajibu kutimiza?
Mapambo
yanazidia, na gharama zazidia,
Hesabu
ukijakupewa, kijiji kingelipaa,
Kama
Ulaya kikawa, pasenti kingelipewa,
Unataka
kusifiwa, kwa wajibu kutimiza?
Na
safari za kuzua, mtu usipotulia,
Wala
kazi kuizua, matunda itayozaa,
Linanizidi
butwaa, utani ninajionea,
Unataka
kusifiwa, kwa wajibu kutimiza?
Mwaweza
kunichukia, ukweli sintouua,
Daima
nitautoa, chama kilishanambia,
Matapishi
kurejea, kula kwangu haijawa,
Unataka
kusifiwa, kwa wajibu kutimiza?
Ibilisi
kaingia, wafuasi achezea,
Ya
ovyo tunayazua, chama yasiyosidia,
Aibu
tusipojua, kuaibika tabia,
Unataka
kusifiwa, kwa wajibu kutimiza?
Kila
tunalolizua, na sisi tutazuliwa,
Kashfa
mbona balaa, makapuni zimejaa,
Muda
unasubiriwa, uvundo kuuachia,
Unataka
kusifiwa, kwa wajibu kutimiza?
Wa
mwenzio 'sipomlea, wako hatatengemaa,
Wapi
ulijionea, salama linalokuwa,
Shamba
lililokaribia, gugu linapoachiwa ?
Unataka
kusifiwa, kwa wajibu kutimiza?
Mharibu
cha jamaa, chake kitharibiwa,
Kila
mpenda ubaya, ubaya humfatia,
Ila
kheri mkimbilia, kheri itamlilia,
Unataka
kusifiwa, kwa wajibu kutimiza?
No comments:
Post a Comment