Saturday, February 25, 2012
Lugha ya watu mizizi
Lugha wanajivunia, hata kidogo wakiwa,
Nyengine kutotumia, ila nje wanapokuwa,
Lugha ya watu mizizi, ikikatwa mti hufa:
Au ikifukuliwa
Na pengine kung'olewa
Utamaduni huvia
Taifa lije lemaa
Asili ikapotea
Uvumbuzi nao pia
Watu wabakie kuwa
Vya wengine watumia
Pasiwe kitu kimoya
Wao wanachogundua!
Chao wanajivunia, bila ya kusimamiwa,
Na kisha waongezea, vya wengine kuvijua,
Ubingwa kujipatia, kwayo na yale ya dunia,
Lugha ya watu mizizi, ikikatwa mti hufa:
Au ikifukuliwa
Na pengine kung'olewa
Utamaduni huvia
Taifa lije lemaa
Asili ikapotea
Uvumbuzi nao pia
Watu wabakie kuwa
Vya wengine watumia
Pasiwe kitu kimoya
Wao wanachogundua!
Asili waangalia, urithi kutopotea,
Pia rahisi ikawa, watoto kujifunzia,
Lughani wakichipua, mengi sana huyajua,
Lugha ya watu mizizi, ikikatwa mti hufa:
Au ikifukuliwa
Na pengine kung'olewa
Utamaduni huvia
Taifa lije lemaa
Asili ikapotea
Uvumbuzi nao pia
Watu wabakie kuwa
Vya wengine watumia
Pasiwe kitu kimoya
Wao wanachogundua!
Leo hapa Tanzania, maneno yanapotea,
Ndege wetu kuwajua, wazima utawaumbua,
Sembese watoto kuwa, hawana wanalojua,
Lugha ya watu mizizi, ikikatwa mti hufa:
Au ikifukuliwa
Na pengine kung'olewa
Utamaduni huvia
Taifa lije lemaa
Asili ikapotea
Uvumbuzi nao pia
Watu wabakie kuwa
Vya wengine watumia
Pasiwe kitu kimoya
Wao wanachogundua!
Wanyama nao pia, wawili watatu wajua,
Samaki waliojaa, bahari nayo maziwa,
Wangapi watakwambia, majina waliyopewa?
Lugha ya watu mizizi, ikikatwa mti hufa:
Au ikifukuliwa
Na pengine kung'olewa
Utamaduni huvia
Taifa lije lemaa
Asili ikapotea
Uvumbuzi nao pia
Watu wabakie kuwa
Vya wengine watumia
Pasiwe kitu kimoya
Wao wanachogundua!
Miti na mingi mimea, hakuna anayejua,
Utacheka nakwambia, mjini ukiulizia,
Afadhali inakuwa, kijijini wanajua,
Lugha ya watu mizizi, ikikatwa mti hufa:
Au ikifukuliwa
Na pengine kung'olewa
Utamaduni huvia
Taifa lije lemaa
Asili ikapotea
Uvumbuzi nao pia
Watu wabakie kuwa
Vya wengine watumia
Pasiwe kitu kimoya
Wao wanachogundua!
Maumbo yake dunia, wengi utata hukuwa,
Bure utajisumbua, hakuna anayejua,
Na hawa wategemea, kitu kuja kuvumbua?
Lugha ya watu mizizi, ikikatwa mti hufa:
Au ikifukuliwa
Na pengine kung'olewa
Utamaduni huvia
Taifa lije lemaa
Asili ikapotea
Uvumbuzi nao pia
Watu wabakie kuwa
Vya wengine watumia
Pasiwe kitu kimoya
Wao wanachogundua!
Mizizi yake mmea, asili hutegemea,
Ndipo inapokuwa, kwa yote yanayokuwa,
Elimu ikiwa pia, muhimu kuzingatiwa,
Lugha ya watu mizizi, ikikatwa mti hufa:
Au ikifukuliwa
Na pengine kung'olewa
Utamaduni huvia
Taifa lije lemaa
Asili ikapotea
Uvumbuzi nao pia
Watu wabakie kuwa
Vya wengine watumia
Pasiwe kitu kimoya
Wao wanachogundua!
Watafeli nadharia, kwa lugha kutoijua,
Watoto kuwakandia, ya uongo yalokuwa,
Walimu kuwazulia, hata wasiyofikiria,
Lugha ya watu mizizi, ikikatwa mti hufa:
Au ikifukuliwa
Na pengine kung'olewa
Utamaduni huvia
Taifa lije lemaa
Asili ikapotea
Uvumbuzi nao pia
Watu wabakie kuwa
Vya wengine watumia
Pasiwe kitu kimoya
Wao wanachogundua!
Kiswahili kutumia, kufundisha nadharia,
Kwa undani kuelewa, yote yanayozungumziwa,
Haya wakishayajua, Kama China tutakuwa,
Lugha ya watu mizizi, ikikatwa mti hufa:
Au ikifukuliwa
Na pengine kung'olewa
Utamaduni huvia
Taifa lije lemaa
Asili ikapotea
Uvumbuzi nao pia
Watu wabakie kuwa
Vya wengine watumia
Pasiwe kitu kimoya
Wao wanachogundua!
Tuitenge nadharia, na lugha kufundishia,
Maabara kufungua, shuleni na vyuo pia,
Lugha kuzikazania, mbili tatu wakajua,
Lugha ya watu mizizi, ikikatwa mti hufa:
Au ikifukuliwa
Na pengine kung'olewa
Utamaduni huvia
Taifa lije lemaa
Asili ikapotea
Uvumbuzi nao pia
Watu wabakie kuwa
Vya wengine watumia
Pasiwe kitu kimoya
Wao wanachogundua!
Ndege wengi tutaua,kwa jiwe moja kutumia,
Sayansi wakaijua, na lugha kuzing'amua,
Hata Kiarabu pia, na Kichina kutumia,
Lugha ya watu mizizi, ikikatwa mti hufa:
Au ikifukuliwa
Na pengine kung'olewa
Utamaduni huvia
Taifa lije lemaa
Asili ikapotea
Uvumbuzi nao pia
Watu wabakie kuwa
Vya wengine watumia
Pasiwe kitu kimoya
Wao wanachogundua!
Mashariki inafaa, tuanze kuangalia,
Isiwe tunachelewa,
Wenzeetu wakatangulia,
Lugha yetu kujitia, lakini kutokutufaa,
Lugha ya watu mizizi, ikikatwa mti hufa:
Au ikifukuliwa
Na pengine kung'olewa
Utamaduni huvia
Taifa lije lemaa
Asili ikapotea
Uvumbuzi nao pia
Watu wabakie kuwa
Vya wengine watumia
Pasiwe kitu kimoya
Wao wanachogundua!
Viongozi watakiwa, uzito kuuchukua,
Wafanze kuyaamua, mapema inavyokuwa,
Nami sintoshangaa, wengine kutangulia,
Lugha ya watu mizizi, ikikatwa mti hufa:
Au ikifukuliwa
Na pengine kung'olewa
Utamaduni huvia
Taifa lije lemaa
Asili ikapotea
Uvumbuzi nao pia
Watu wabakie kuwa
Vya wengine watumia
Pasiwe kitu kimoya
Wao wanachogundua!
Kiingereza balaa, ujanja wanatumia,
Lugha yetu kuiua, na yao kuendlea,
Na sisi kamamajuha, mtegoni twaingia,
Lugha ya watu mizizi, ikikatwa mti hufa:
Au ikifukuliwa
Na pengine kung'olewa
Utamaduni huvia
Taifa lije lemaa
Asili ikapotea
Uvumbuzi nao pia
Watu wabakie kuwa
Vya wengine watumia
Pasiwe kitu kimoya
Wao wanachogundua!
Nyerere alianzia, lugha kasaliti pia,
Mwinyi alipofatia, naye akazainiwa,
Mkapa hakujitambua, wala hatajitambua,
Lugha ya watu mizizi, ikikatwa mti hufa:
Au ikifukuliwa
Na pengine kung'olewa
Utamaduni huvia
Taifa lije lemaa
Asili ikapotea
Uvumbuzi nao pia
Watu wabakie kuwa
Vya wengine watumia
Pasiwe kitu kimoya
Wao wanachogundua!
Kikwete asipojua, humo humo kufatia,
Kiswahili kukiua, na elimu nayo pia,
Ndicho kilichobakia, na ndiyo yanayotokea,
Lugha ya watu mizizi, ikikatwa mti hufa:
Au ikifukuliwa
Na pengine kung'olewa
Utamaduni huvia
Taifa lije lemaa
Asili ikapotea
Uvumbuzi nao pia
Watu wabakie kuwa
Vya wengine watumia
Pasiwe kitu kimoya
Wao wanachogundua!
Ila mtunzi najua, rais wa Tanzania,
Kweli atakayekuwa, Kiswahili ataamua,
Kila ngazi kutumia, na nchi ikaendelea,
Lugha ya watu mizizi, ikikatwa mti hufa:
Au ikifukuliwa
Na pengine kung'olewa
Utamaduni huvia
Taifa lije lemaa
Asili ikapotea
Uvumbuzi nao pia
Watu wabakie kuwa
Vya wengine watumia
Pasiwe kitu kimoya
Wao wanachogundua!
Kwenye kapu watupiwa, wote waliotangulia,
Takataka watakuwa, kati yetu historia,
Nafasi waliipewa, ila hawakuitumia,
Lugha ya watu mizizi, ikikatwa mti hufa:
Au ikifukuliwa
Na pengine kung'olewa
Utamaduni huvia
Taifa lije lemaa
Asili ikapotea
Uvumbuzi nao pia
Watu wabakie kuwa
Vya wengine watumia
Pasiwe kitu kimoya
Wao wanachogundua!
Kuthubutu hapakua, na kujaribu wapwaya,
Hakuna walilojaliwa, kuliweza na kujua,
Waigaji wabakia, ni wasanii bandia,
Lugha ya watu mizizi, ikikatwa mti hufa:
Au ikifukuliwa
Na pengine kung'olewa
Utamaduni huvia
Taifa lije lemaa
Asili ikapotea
Uvumbuzi nao pia
Watu wabakie kuwa
Vya wengine watumia
Pasiwe kitu kimoya
Wao wanachogundua!
Unajifanya usilokuwa ?
Ijapo nafasi ulishaipewa
Kiumbe jema hukujaliwa
Ila mabaya umeumbiwa
Shetani amekuchukuwa
Kama kifaa unatumiwa
Naye si rahisi ukajaliwa
Minyororoni ukajitowa
Yawa kama umelaniwa
Kwa pako pema kukimbiwa
Ukakimbilia kwenye mabaya!
Wajifanya usilokuwa
Nuksi hapo ndio zaanzia!
Umeme unapozima
Kwenye nchi ya madoa, rangi tusiyoyajua,
Na amri za kuua, wadhani hawajaua,
Na yatakiwayo kuwa, yasiwe yenye kukua,
Umeme unapozima, na giza likaenea:
Mwangaza hunifunua,
Utunzi nikaingia,
Hadi adhana ikawa!
Ukuu wanaochukua, wasiwe pakuanzia,
Na wanaoyachimbua, wakadhani walimia,
Huwa nchi ya wafukua, kuzikwa kwao haijawa,
Umeme unapozima, na giza likaenea:
Mwangaza hunifunua,
Utunzi nikaingia,
Hadi adhana ikawa!
Ndipo saa wazijua, kizani kutususia,
Mengi yananipitia, pembeni nilipokaa,
Wasiojua wajua, ndiyo nchi imekuwa,
Umeme unapozima, na giza likaenea:
Mwangaza hunifunua,
Utunzi nikaingia,
Hadi adhana ikawa!
Hakuna wa kutumiwa, wote wataka tumia,
Kuvuna washangilia, kupanda wanakataa,
Wachache hupalilia, nao mimea hung'oa,
Umeme unapozima, na giza likaenea:
Mwangaza hunifunua,
Utunzi nikaingia,
Hadi adhana ikawa!
Nchi ya wasiojijua, na kwendako wapotea,
Taifa lisilojifua, kutakata haijawa,
Na uchafu waujua, tena wanautumia,
Umeme unapozima, na giza likaenea:
Mwangaza hunifunua,
Utunzi nikaingia,
Hadi adhana ikawa!
Watu wa kusaidiwa, wasiojisaidia,
Nchi yenye kununua, chake isichokizaa,
Ni nchi ya kulaniwa, mbele haitoendelea,
Umeme unapozima, na giza likaenea:
Mwangaza hunifunua,
Utunzi nikaingia,
Hadi adhana ikawa!
Nchi ya viguu na njia, haiwezi kutulia,
Yao wasiotatua, ya wengine wakavaa,
Ni ya kusikitikiya, na tena kuhurumiwa,
Umeme unapozima, na giza likaenea:
Mwangaza hunifunua,
Utunzi nikaingia,
Hadi adhana ikawa!
Ndio ninafurahia, umeme ukisinzia,
Huamka na kuzua, visa vya kuhadithia,
Kizazi kitachokuwa, haya kuja yaambaa,
Umeme unapozima, na giza likaenea:
Mwangaza hunifunua,
Utunzi nikaingia,
Hadi adhana ikawa!
Binadamu si mashine
Hukuumbwa mashine, binadamu nakwambia,
Wapaswa kujitambua, akili kuitumia,
Watu wakikutumia, unakuwa ni kifaa,
Binadamu si mashine, apaswa kufikiria!
Itihari kajaliwa, kupima na kuchagua,
Afanye linalofaa, muktadha kuujua,
Na haki kuzingatia, kazini anapokuwa,
Binadamu si mashine, anapaswa kuchagua!
Ubongo kazawadiwa, apaswa kuutumia,
Na akishajipimia, mwenyewe akaamua,
Kwa vigezo vilokuwa, na watu na matukio,
Binadamu si mashine, anapaswa kuamua!
Vinginevyo ni bandia, mwanasesere akawa,
Wawe wamchezea, juu walotangulia,
Dhambi kumuachia, mwenyewe kujibebea,
Binadamu si mashine, apaswa kufikiria!
Wanasiasa balaa, fani
Watu shere watezea,
Ikawa wawakubalia, hata kwa yasiyokuwa,
Binadamu si mashine, anapaswa kuchagua!
Enzi zimeshaingia, watu kujiangalia,
Uhuru wakachagua, na haki kuzingatia,
Pasiwe wa kutumiwa, hadaa na kuzainiwa,
Binadamu si mashine, anapaswa kuamua!
Usitende bila fikra
Mnyama ungelikuwa, sawa tungelidhania,
Mambo kutofikiria, na kisha ukayaingia,
Utu yende kukuvua, na uchi ukabakia,
Usitende bila fikra, waza kabla kutenda!
Fikra ni majaliw,a mja amezawadiwa,
Yafaa kufikiria, kabla haujaamua,
Na utenzi hutanguliwa, kwa mawazo yalokuwa,
Usitende bila fikra, waza kabla kutenda!
Amri kuzipokea, ukatenda usojua,
Wewe umelaaniwa, na mbingu na ardhi pia,
Na moto wa kungojea, hunalo la kujitetea,
Usitende bila fikra, waza kabla kutenda!
La haki lililokuwa, kulitenda inafaa,
Na haki lisilokuwa, ni wajibu kukataa,
Muogopeni Jalia, si watu kuwahofia,
Usitende bila fikra, waza kabla kutenda!
Watu wao wapigao
Ukubwa wautakao, wale wao na wakwao,
Walinzi wafugwao, kulinda wakubwa wao,
Watu wao wapigao, si amani watakao!
Hudhani wao ni wao, na nchi hii ni
Katiba wapinduao, juu kujiweka wao,
Na wananchi walalao, wakawa nalo pumbao,
Watu wao wapigao, si amani watakao!
Wasijue kuwa wao, ndio wao wafukuzao,
Asibaki mmojawao, zahama ikija kwao,
Uwe ni mwisho wao, na mwanzo wa wajuao,
Watu wao wapigao, si amani watakao!
Sauti ni nyie mnayo, na mambo muamuoa,
Mkitaka watoke wao, kutoka lazima kwao,
Isiwe ni warudio, juu tena sio yao,
Watu wao wapigao, si amani watakao!
Ni nyie muwawekao, na muamalizao,
Kwa lenu moja amuo, watoke hapo si kwao,
Wako wengi wenzao, nafasi waitakayo,
Watu wao wapigao, si amani watakao!
Haitoshi wajivuao, gamba liozalo kwao,
Na ngozi yenye kumbao, mwilini wabakiayo,
Uchago hulia wao, waulaliapo mwao,
Watu wao wapigao, si amani watakao!
Naamba niwaambiao, nyakati hizi si zao,
Mabadiliko ni ngao, huvunjika zao tao,
Yajayo si wazuiayo, watatoka watokao,
Watu wao wapigao, si amani watakao!
Kivumbasi mwanakwao, heri si wajaliwao,
Shetani ana kikao, mara kwa mara nao,
Na haya waamuayo, mwayaona yazuayo,
Watu wao wapigao, si amani watakao!
Urithi si watakao, wawapa kwanza wanao,
Kuua ni jadi
Mti hujazaa mbao, si mbao yenye uzao,
Watu wao wapigao, si amani watakao!
Walioshindwa mbinu
Mbinu walioishiwa, wepesi kukimbilia,
Fujo kuzichochea, wavune yanayowafaa,
Ukubwa kuutetea, japo waisha raia,
Walioshindwa mbinu, mikakati na fikra:
Mabavu huyatumia!
Ni watu wa kuteua, watu wasiowafaa,
Yao waangalia, si ya wengi yakawa,
Ni laana tumeachiwa, bado tunaing'ang'ania,
Walioshindwa mbinu, mikakati na fikra:
Mabavu huyatumia!
Enzi za kutofikiria, ukingoni zafikia,
Watu wataulizia, hata yale yasokuwa,
Na wajibu kuwatia, wajifanyao wajua,
Walioshindwa mbinu, mikakati na fikra:
Mabavu huyatumia!
Majoho watawavua, yafichyo kuishiwa,
Ujinga wakawaachia, na wengine kuchagua,
Pasiwe wa kubakia, na mtu anayetumiwa,
Walioshindwa mbinu, mikakati na fikra:
Mabavu huyatumia!
Unapojenga chuki
Nani aliyewatuma, au kisasi mwatukua,
Nahisi kuna nakama, hawajui wasojua,
Unapojenga chuki, kwa polisi na raia:
Taifa unaliua,
Umoja unaambaa,
Na amani yapotea!
Zana mnazozifuma, vitani zilitakiwa,
Au migodi kuchuma, hicho kinachoibiwa,
Sio kuutesa umma, na uyatima kwingia,
Unapojenga chuki, kwa polisi na raia:
Taifa unaliua,
Umoja unaambaa,
Na amani yapotea!
Mwaturudisha nyuma, juu mliotangulia,
Na busara na hekima, yawa kama isokuwa,
Ni mashaka na tuhuma, nyuma yanawafatia,
Unapojenga chuki, kwa polisi na raia:
Taifa unaliua,
Umoja unaambaa,
Na amani yapotea!
Mambo yataka kalima, si magomvi kuyazua,
Utu usio heshima, haikubali dunia,
Hata mtumie vyuma, haki itapiganiwa,
Unapojenga chuki, kwa polisi na raia:
Taifa unaliua,
Umoja unaambaa,
Na amani yapotea!
Mwatia watu ulema, ndani waliotulia,
Na uongo kuusema, deraya wanavamia,
Hachagui la kusema, muongo alolaaniwa,
Unapojenga chuki, kwa polisi na raia:
Taifa unaliua,
Umoja unaambaa,
Na amani yapotea!
Nchi yataka adhama, watu waliojaliwa,
Wenye kuwa roho njema, na uhai kuulea,
Si wenye kuwasakama, hatia wasiokuwa,
Unapojenga chuki, kwa polisi na raia:
Taifa unaliua,
Umoja unaambaa,
Na amani yapotea!
Mkoloni anasema, mbinu zetumia,
Dhidi ya kwao umma, kama tulivyoanzia,
Ni ipi yao heshima, kulikoni tulokuwa?
Unapojenga chuki, kwa polisi na raia:
Taifa unaliua,
Umoja unaambaa,
Na amani yapotea!
Weupe watusakama, weusi wameingia,
Feli na zao kalima, yale yale yamekuwa,
Dunia hii sinema, na mcheza utamjua!
Unapojenga chuki, kwa polisi na raia:
Taifa unaliua,
Umoja unaambaa,
Na amani yapotea!
Mola wetu muadhama, tabia aichukia,
Na wasio na hekima, kwenu kujipalilia,
Wakidai mwendo nyuma, bei
Unapojenga chuki, kwa polisi na raia:
Taifa unaliua,
Umoja unaambaa,
Na amani yapotea!
Gari wamwachia nani?
GARI uliowachia, kuendesha wanajua?
Au sukani waachia, frii kujiendea?
Ajali naingojea, siku nyingi haitokuwa,
Kaka yangu nauliza, kwenda nje wapania:
Nyumba wamwachia nani,
Jamaa wako salama?
Basi lako waachia, la wengine wadandia,
Suka ajabu watoa, watu wanakushangaa,
Konda amedandia, kuendesha hajajua,
Kaka yangu nauliza, kwenda nje wapania:
Nyumba wamwachia nani,
Jamaa wako salama?
Mkuu anangojewa, kwenye kiti keshakaa,
Mbona rivasi atia, badala moja kutia,
Bonde nyuma limekaa, na kiama chatujia,
Kaka yangu nauliza, kwenda nje wapania:
Nyumba wamwachia nani,
Jamaa wako salama?
Deiwaka wamejaa, mikoa hadi wilaya,
Kila siku twasikiya, mashimo wanavyoingia,
Kujiamini sanaa, na mafao si kufaa,
Kaka yangu nauliza, kwenda nje wapania:
Nyumba wamwachia nani,
Jamaa wako salama?
Wanashiba wenye njaa, mlo wakishaupewa,
Ila yaja kubakia, wenye njaa watawajua?
Nani wa kujitendea, yeye anayoamua,
Kaka yangu nauliza, kwenda nje wapania:
Nyumba wamwachia nani,
Jamaa wako salama?
Na mkuu wa mkoa, ambaye huteuliwa,
Aweza lea raia, au nguvu atumia,
Fimbo ndogo limekua, sasa gogo kakamia ?
Kaka yangu nauliza, kwenda nje wapania:
Nyumba wamwachia nani,
Jamaa wako salama?
Gari lisilodhibitiwa, liendako hutojua,
Huwa ni
Na ndivyo inavyokuwa, na yote tunayajua,
Kaka yangu nauliza, kwenda nje wapania:
Nyumba wamwachia nani,
Jamaa wako salama?
Gari wakiachiwa, kuendesha wasojua,
Huishiwa abiria, amani ikapotea,
Akabaki kulia, yarabi kumuokoa,
Kaka yangu nauliza, kwenda nje wapania:
Nyumba wamwachia nani,
Jamaa wako salama?
Na mkuu wa wilaya, watu wake awajua,
Au kazi kusakazia, raia wakaratua,
Na vibaka kuingia, hata nje walokuwa,
Kaka yangu nauliza, kwenda nje wapania:
Nyumba wamwachia nani,
Jamaa wako salama?
Kamanda waliopewa, ni kina Mabula pawa,
Au busara wapewa, kihaki kuyaamua,
Na siyo ya kufokewa, na amri za umbeya?
Kaka yangu nauliza, kwenda nje wapania:
Nyumba wamwachia nani,
Jamaa wako salama?
Na waziri
Afanze ya kumfaa, kwa wengine kiama kuwa,
Bila kufuatilia, nchi haitopotea?
Kaka yangu nauliza, kwenda nje wapania:
Nyumba wamwachia nani,
Jamaa wako salama?
Miundo iliyokuwa, watu geti wakataa,
Inapaswa kufungua, uhuru watu wakawa,
La sivyo yatatokea, kwingine yanayotokea,
Kaka yangu nauliza, kwenda nje wapania:
Nyumba wamwachia nani,
Jamaa wako salama?
Mifumo watu wafumua, yawabana kifua,
Na miundo waezua, madirisha kupanua,
Na milango kuitia, mikubwa iliyokuwa,
Kaka yangu nauliza, kwenda nje wapania:
Nyumba wamwachia nani,
Jamaa wako salama?
Wewe ukiendelea, mlangoni kuzuia,
Waktioka wakatua, hapo ulipotegea,
Pembeni watakufagia, mbele wende angukia,
Kaka yangu nauliza, kwenda nje wapania:
Nyumba wamwachia nani,
Jamaa wako salama?
Yanayotokea Mbeya, Arusha nako Songea,
Ujumbe nausikia, nawe haujasikia?
Mikoa huru ikiwa, balaa tutaambaa,
Kaka yangu nauliza, kwenda nje wapania:
Nyumba wamwachia nani,
Jamaa wako salama?
Kuzidi kung'ang'ania, mabaa yakaribia,
Hakuna la kujivua, kwa wingi tutaangamia,
Tunaishindwa mikoa, tutaiweza
Kaka yangu nauliza, kwenda nje wapania:
Nyumba wamwachia nani,
Jamaa wako salama?
Kumpanda mume la'na, na sasa unayaona!
Na nilikuangalia, na kutaka kukulea,
Mjinga kwako nikawa, na kubasi la kwogea,
Yangu uliyakataa, ya ngoroko kuchukua,
Kumpanda mume la'na, na sasa unayaona!
Jeui ukajitia, na matusi kukujaa,
Dharau ukaivaa, na shanga kuivalia,
Nami kimya nikakaa, siku nikiingojea,
Kumpanda mume la'na, na sasa unayaona!
Muda haukuchelewa, miaka ikafikia,
Uhuru ulipokuwa, na waoto wamekua,
Hukujua nangojea, ulidhani natania,
Kumpanda mume la'na, na sasa unayaona!
Ulikuwa ni kichaa, mtu usiyesikia,
Yako kujifanyia, yasiyowapendezea,
Na laana kufukua, na wana kuwatupia,
Kumpanda mume la'na, na sasa unayaona!
Mapenzi hukujaliwa, ila wabeba sanaa,
Kila kitu kujitia, wajua usiyejua,
Wengi wakakushangaa, ujinga uliovaa,
Kumpanda mume la'na, na sasa unayaona!
Juzuu kukazania, sasa unattakiwa,
Sura Na'ba kuijua, dua ukaiombea,
Maradhi kukupungua, kichwani yalokujaa,
Kumpanda mume la'na, na sasa unayaona!
Na jeneza kuzuia, wana lisije chukua,
Wazee wako yafaa, kinga kuwaulizia,
Upuuzi uliotoa, madhara kutotokea,
Kumpanda mume la'na, na sasa unayaona!
Ni mpweke nitakuwa, ila kensa naitoa,
Pengine nitafikiria, madeni ukilipiwa,
Nyumbani ukarejea, mama wa nyumbani kuwa,
Kumpanda mume la'na, na sasa unayaona!
Biashara nakataa, marufuku kuijua,
Ila vitu kuandaa, nyumbani unapokuwa,
Na mikopo kuchukua, si ruhusa nakwambia,
Kumpanda mume la'na, na sasa unayaona!
Wataka waharibia, wana wangali wakua,
Msingi kumalizia, chini wote kuishia,
Hakika wakosa haya, kisirani umekuwa,
Kumpanda mume la'na, na sasa unayaona!
Na jeuri wajitia, kujifanya waonewa,
Mwisho umeshafikia, ukweli tunaujua,
Wengi umewaibia, siku zote wanalia,
Kumpanda mume la'na, na sasa unayaona!
Nakuomba angukia, ndugu kukusaidia,
Mikopo uliyochukua, na wizi ulokuwa,
Madeni kukulipia, salama upate kuwa,
Kumpanda mume la'na, na sasa unayaona!
Dharau imekuponza
Na nilikuangalia, na kutaka kukulea,
Mjinga kwako nikawa, na kubasi la kuvua,
Yangu uliyakataa, ya ngoroko kuchukua,
Dharau imekuponza, sasa wajidhalilisha!
Jeui ukajitia, na matusi kukujaa,
Dharau ukaivaa, na shanga kuivalia,
Nami kimya nikakaa, siku nikiingojea,
Dharau imekuponza, sasa wajidhalilisha!
Muda haukuchelewa, miaka ikafikia,
Uhuru ulipokuwa, na waoto wamekua,
Hukujua nangojea, ulidhani natania,
Dharau imekuponza, sasa wajidhalilisha!
Ulikuwa ni kichaa, mtu usiyesikia,
Yako kujifanyia, yasiyowapendezea,
Na laana kufukua, na wana kuwatupia,
Dharau imekuponza, sasa wajidhalilisha!
Mapenzi hukujaliwa, ila wabeba sanaa,
Kila kitu kujitia, wajua usiyejua,
Wengi wakakushangaa, ujinga uliovaa,
Dharau imekuponza, sasa wajidhalilisha!
Juzuu kukazania, sasa unattakiwa,
Sura Na'ba kuijua, dua ukaiombea,
Maradhi kukupungua, kichwani yalokujaa,
Dharau imekuponza, sasa wajidhalilisha!
Na jeneza kuzuia, wana lisije chukua,
Wazee wako yafaa, kinga kuwaulizia,
Upuuzi uliotoa, madhara kutotokea,
Dharau imekuponza, sasa wajidhalilisha!
Ni mpweke nitakuwa, ila kensa naitoa,
Pengine nitafikiria, madeni ukilipiwa,
Nyumbani ukarejea, mama wa nyumbani kuwa,
Dharau imekuponza, sasa wajidhalilisha!
Biashara nakataa, marufuku kuijua,
Ila vitu kuandaa, nyumbani unapokuwa,
Na mikopo kuchukua, si ruhusa nakwambia,
Dharau imekuponza, sasa wajidhalilisha!
Wataka waharibia, wana wangali wakua,
Msingi kumalizia, chini wote kuishia,
Hakika wakosa haya, kisirani umekuwa,
Dharau imekuponza, sasa wajidhalilisha!
Na jeuri wajitia, kujifanya waonewa,
Mwisho umeshafikia, ukweli tunaujua,
Wengi umewaibia, siku zote wanalia,
Dharau imekuponza, sasa wajidhalilisha!
Nakuomba angukia, ndugu kukusaidia,
Mikopo uliyochukua, na wizi ulokuwa,
Madeni kukulipia, salama upate kuwa,
Dharau imekuponza, sasa wajidhalilisha!
Kiburi kimekuponza,
Na nilikuangalia, na kutaka kukulea,
Mjinga kwako nikawa, na kubasi la kuvua,
Yangu uliyakataa, ya ngoroko kuchukua,
Kiburi kimekuponza, mbona sasa unalia ?
Jeui ukajitia, na matusi kukujaa,
Dharau ukaivaa, na shanga kuivalia,
Nami kimya nikakaa, siku nikiingojea,
Kiburi kimekuponza, mbona sasa unalia ?
Muda haukuchelewa, miaka ikafikia,
Uhuru ulipokuwa, na waoto wamekua,
Hukujua nangojea, ulidhani natania,
Kiburi kimekuponza, mbona sasa unalia ?
Ulikuwa ni kichaa, mtu usiyesikia,
Yako kujifanyia, yasiyowapendezea,
Na laana kufukua, na wana kuwatupia,
Kiburi kimekuponza, mbona sasa unalia ?
Mapenzi hukujaliwa, ila wabeba sanaa,
Kila kitu kujitia, wajua usiyejua,
Wengi wakakushangaa, ujinga uliovaa,
Kiburi kimekuponza, mbona sasa unalia ?
Juzuu kukazania, sasa unattakiwa,
Sura Na'ba kuijua, dua ukaiombea,
Maradhi kukupungua, kichwani yalokujaa,
Kiburi kimekuponza, mbona sasa unalia ?
Na jeneza kuzuia, wana lisije chukua,
Wazee wako yafaa, kinga kuwaulizia,
Upuuzi uliotoa, madhara kutotokea,
Kiburi kimekuponza, mbona sasa unalia ?
Ni mpweke nitakuwa, ila kensa naitoa,
Pengine nitafikiria, madeni ukilipiwa,
Nyumbani ukarejea, mama wa nyumbani kuwa,
Kiburi kimekuponza, mbona sasa unalia ?
Biashara nakataa, marufuku kuijua,
Ila vitu kuandaa, nyumbani unapokuwa,
Na mikopo kuchukua, si ruhusa nakwambia,
Kiburi kimekuponza, mbona sasa unalia ?
Wataka waharibia, wana wangali wakua,
Msingi kumalizia, chini wote kuishia,
Hakika wakosa haya, kisirani umekuwa,
Kiburi kimekuponza, mbona sasa unalia ?
Na jeuri wajitia, kujifanya waonewa,
Mwisho umeshafikia, ukweli tunaujua,
Wengi umewaibia, siku zote wanalia,
Kiburi kimekuponza, mbona sasa unalia ?
Nakuomba angukia, ndugu kukusaidia,
Mikopo uliyochukua, na wizi ulokuwa,
Madeni kukulipia, salama upate kuwa,
Kiburi kimekuponza, mbona sasa unalia ?
Jeuri imekuponza
Na nilikuangalia, na kutaka kukulea,
Mjinga kwako nikawa, na kubasi la kuvua,
Yangu uliyakataa, ya ngoroko kuchukua,
Jeuri imekuponza, mwenyewe wajiumiza!
Jeui ukajitia, na matusi kukujaa,
Dharau ukaivaa, na shanga kuivalia,
Nami kimya nikakaa, siku nikiingojea,
Jeuri imekuponza, mwenyewe wajiumiza!
Muda haukuchelewa, miaka ikafikia,
Uhuru ulipokuwa, na waoto wamekua,
Hukujua nangojea, ulidhani natania,
Jeuri imekuponza, mwenyewe wajiumiza!
Ulikuwa ni kichaa, mtu usiyesikia,
Yako kujifanyia, yasiyowapendezea,
Na laana kufukua, na wana kuwatupia,
Jeuri imekuponza, mwenyewe wajiumiza!
Mapenzi hukujaliwa, ila wabeba sanaa,
Kila kitu kujitia, wajua usiyejua,
Wengi wakakushangaa, ujinga uliovaa,
Jeuri imekuponza, mwenyewe wajiumiza!
Juzuu kukazania, sasa unattakiwa,
Sura Na'ba kuijua, dua ukaiombea,
Maradhi kukupungua, kichwani yalokujaa,
Jeuri imekuponza, mwenyewe wajiumiza!
Na jeneza kuzuia, wana lisije chukua,
Wazee wako yafaa, kinga kuwaulizia,
Upuuzi uliotoa, madhara kutotokea,
Jeuri imekuponza, mwenyewe wajiumiza!
Ni mpweke nitakuwa, ila kensa naitoa,
Pengine nitafikiria, madeni ukilipiwa,
Nyumbani ukarejea, mama wa nyumbani kuwa,
Jeuri imekuponza, mwenyewe wajiumiza!
Biashara nakataa, marufuku kuijua,
Ila vitu kuandaa, nyumbani unapokuwa,
Na mikopo kuchukua, si ruhusa nakwambia,
Jeuri imekuponza, mwenyewe wajiumiza!
Wataka waharibia, wana wangali wakua,
Msingi kumalizia, chini wote kuishia,
Hakika wakosa haya, kisirani umekuwa,
Jeuri imekuponza, mwenyewe wajiumiza!
Na jeuri wajitia, kujifanya waonewa,
Mwisho umeshafikia, ukweli tunaujua,
Wengi umewaibia, siku zote wanalia,
Jeuri imekuponza, mwenyewe wajiumiza!
Nakuomba angukia, ndugu kukusaidia,
Mikopo uliyochukua, na wizi ulokuwa,
Madeni kukulipia, salama upate kuwa,
Jeuri imekuponza, mwenyewe wajiumiza!
Kuiga mambo ya watu
Akili hukutumia, ingwa umejaliwa,
Bahati ukachezea, chooni ulipokuwa,
Shilingi kutumbukia, vyote vimeshapotea,
Kufata watu wa nje, wa ndani ukawabeza:
Nyongo yakutumbukia!
Ya mme hukusikia, kiburi ukajitia,
Na jeuri ukawa, kila alipokuongoa,
Heri ukaikataa, na shari kukurubia,
Kufata watu wa nje, wa ndani ukawabeza:
Nyongo yakutumbukia!
Wa nje kuwaendea, shirika kujifanyia,
Na waganga kuzoea, ushirikina kujaa,
Mkawa mwachanganyikiwa, mwazidi potea njia,
Kufata watu wa nje, wa ndani ukawabeza:
Nyongo yakutumbukia!
Wakowapi walokua, kila siku wasifia,
Kidume uliyekuwa, mume chini yako kawa,
Kumbe akuhesabia, siku yako kufikia,
Kufata watu wa nje, wa ndani ukawabeza:
Nyongo yakutumbukia!
Sura ulipuuzia, ila dini wajitia,
Kurani hukuijua, ubishi ulikujaa,
Na ulichoambulia, mwenyewe unakijua,
Kufata watu wa nje, wa ndani ukawabeza:
Nyongo yakutumbukia!
Un afiki kujitia, na uswalihina pia,
Kumbe nyoka ulikua, kichinichini wajia,
Kutuchoma kuamua, nyumbani tulokaa,
Kufata watu wa nje, wa ndani ukawabeza:
Nyongo yakutumbukia!
Dunia yakuumbua, mwanamke wa balaa,
Haya hukuitambua, nani kukuangalia,
Mola ukimrudia, pengine kukuafua,
Kufata watu wa nje, wa ndani ukawabeza:
Nyongo yakutumbukia!
Ushirikina kimbia, au unaangamia,
Na mume kumwangukia, ndiyo dawa itakuwa,
Vinginevyo twachomoa, akhera mbali pia kuwa,
Kufata watu wa nje, wa ndani ukawabeza:
Nyongo yakutumbukia!
Dhuluma kujifanyia, na urushi kuujua,
Sumu yake hukujua, wanao itawavaa,
Wajukuu nao pia, usipowarejeshea,
Kufata watu wa nje, wa ndani ukawabeza:
Nyongo yakutumbukia!
Rahma ungelikuwa, haya yasingetokea,
Ila kwa kukosa neema, ulizaliwa Rehema,
Tubu kisha ungamia,
Kufata watu wa nje, wa ndani ukawabeza:
Nyongo yakutumbukia!
Starehe gani hii ?
Kila mtu ashangaa, dhiki waikimbilia,
Wengi wanavyodhania, pengine umechezewa,
Kulogwa inshakuwa, huu nusu ukichaa,
Starehe gani hii, dhiki kuikimbilia ?
Si bure umechezewa, au mzazi kachukia,
Mema unayotendewa, kwako ubaya inkuwa?
Wengine waililia, nafasi uliyopewa,
Starehe gani hii, dhiki kuikimbilia ?
Uhuru umegaiwa, wewe waudhihakia,
Unaibeza tabia, ya ulua wa kufaa,
Na uchafu wautwaa, mwilini kujimwagiwa,
Starehe gani hii, dhiki kuikimbilia ?
Huu kama ukichaa, naona ilivyokuwa,
Kila siku ikiingia, hali huwa kote mbaya,
Watu wanaulizia, kanyimwa na kupagawa?
Starehe gani hii, dhiki kuikimbilia ?
Wabaya washangilia, zuzu kusesembuliwa,
Raha waitamania, ije kuwaangukia,
Kila wakikazania, kofuli bado yatiwa,
Starehe gani hii, dhiki kuikimbilia ?
Lango langu kufungua, haijawa, nanuia,
Hadi akitokea, malaika atembea,
Urulaini radhia, duniani akajaa,
Starehe gani hii, dhiki kuikimbilia ?
Mazuri wayaachia, mabaya wang'ang'ania,
Nini kinakuzuzua, bado hatujakijua,
Kila pembe twaulizia, majibu hatujapewa,
Starehe gani hii, dhiki kuikimbilia ?
Mtaji umeitwaa, nani kukusaidia,
Wazazi nini kupewa, hali pato umeua?
Wallahi nakusikitia, ninatamani kulia,
Starehe gani hii, dhiki kuikimbilia ?
Raha uliidhania, nje utajiokotea,
Ndani ukapachukia, na wa ndani kuwa udhia,
Laiti ungelijua, ndani ungejiangalia,
Starehe gani hii, dhiki kuikimbilia ?
Siachi kukusetiri
Na mini nakuambia, yako ninahifadhia,
Isipokuwa yalokuwa, nje ya uwezo kuwa,
Siachi kukusetiri, na mini nisetiriwa:
Ila ya wabaya wako, watu lazima kujua,
Hadi radhi kuitoa,
Wakupe na msamaha!
Yako nitakufichia, wengine kutoyajua,
Ila nje uliyotoa, siwezi kuyazuia,
Aibu yako ikawa, mimi haukunambia,
Siachi kukusetiri, na mini nisetiriwa:
Ila ya wabaya wako, watu lazima kujua,
Hadi radhi kuitoa,
Wakupe na msamaha!
Vya watu ulivyotwaa, kurudisha watakiwa,
Laana kutoachiwa, wana wasio hatia,
Mama mpenda familia, hagtotaka kuumia,
Siachi kukusetiri, na mini nisetiriwa:
Ila ya wabaya wako, watu lazima kujua,
Hadi radhi kuitoa,
Wakupe na msamaha!
Watoto unatakiwa, kheri wapate zawadiwa,
Mama kutokuingia, kwenye maovu ya dunia,
Mwenyezi kumrudia, tawba hataoikataa,
Siachi kukusetiri, na mini nisetiriwa:
Ila ya wabaya wako, watu lazima kujua,
Hadi radhi kuitoa,
Wakupe na msamaha!
Shetani alokwingia, pengine atamtoa,
Kawaida kurejea, ibilisi kumwambaa,
Na zako hawa jamaa, salama wakatunukiwa,
Siachi kukusetiri, na mini nisetiriwa:
Ila ya wabaya wako, watu lazima kujua,
Hadi radhi kuitoa,
Wakupe na msamaha!
Nami ninakuombea, tobayo kukubaliwa,
Na rehema ukapewa, na msamaha maridhawa,
Ukaijali familia, pamoja tukarejea,
Siachi kukusetiri, na mini nisetiriwa:
Ila ya wabaya wako, watu lazima kujua,
Hadi radhi kuitoa,
Wakupe na msamaha!