Tuesday, February 14, 2012

Saa ngapi ?

HIVI sasa saa ngapi ?

Nawe umeenda wapi?

Rudi

Njoo

Sasa

Nipo

Peke

Raha

Sina

Wahi ninakungojea

Mkononi uje chanua

Na harufu kuiridhiya

Nitakayo kupumua, sauti ya kusikiya, nyororo ya kutomasa na kizuri cha kuangalia na kukigusa

Ni saa

Kukaa

wawili

Azizi

Pumzi

Kutua

Maisha kuendelea, kupata na kutumia, kupewa na kupokea, kuenzi na kuenziwa, kupenda na ukapendwa

Kawaida ikarejea!!!

Sasa ni saa ngapi ?

No comments: